Tone

Tone
Home » » Usifanye biashara tu, ipangilie kitaalamu

Usifanye biashara tu, ipangilie kitaalamu

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
Mpango wa biashara ni roho ya biashara, kwani ndiyo unaoonyesha dira ya biashara husika. Katika biashara tunasema bila kuwa na mipangilio inayoeleweka, hakuna mafanikio yatakayoonekana.
Mpango wa biashara ni maelezo ya kina yaliyo katika maandishi (na wakati mwingine kichwani mwa mtu) yanayoelezea biashara ya mtu au kampuni fulani.
Maelezo hayo yanahusu bidhaa au huduma za biashara husika, mbinu za uzalishaji, mbinu za kupata masoko, rasirimali watu, muundo wa taasisi, mahitaji ya kifedha ikiwa ni pamoja na vyanzo vyake na matumizi yake.
Mpango wa biashara unaelezea historia ya biashara kwa maana ya wakati uliopita, wakati uliopo na ujao ambayo ndiyo lengo kuu la biashara.
Pamoja na ukweli kuwa kuna mpango wa biashara ambao hauko katika maandishi na ambao hutumiwa na wajasiriamali wadogo walio wengi, katika ulimwengu wa sayansi na teknolojia mpango wa biashara ulio katika maandishi ndiyo unaokubalika zaidi kwani unaweza kushikika na kufuatwa kikamilifu kama mwenye mpango husika atauandaa kwa nia hasa ya kuendeleza biashara yake na wala si tu kwa ajili ya kupata pesa kutoka vyombo vya fedha.
Mpango wa biashara ulio katika maandishi umekuwa ukisisitizwa katika mafunzo mbalimbali yaliyo rasmi kwani unaweza kutumika kuendeshea biashara hata kama mwenye biashara husika hayupo au baada ya kifo cha mmiliki wa biashara au pindi mwenye biasahara apatapo matatizo ya akili.
Kwa kuwa biashara ni maisha ya mjasiriamali na mjasiriamali ni mtu wa mfano katika jamii kutokana na mchango wake katika jamii na taifa kwa ujumla, mpango wa biashara hauna budi kuwa bora ili kutoa picha halisi ya biashara na mmiliki wake.
Mpango mzuri wa biashara una sifa zifuatazo: uliofikiriwa kwa umakini na wenye kutoa picha halisi ya biashara husika, wenye kuelezea ubora na dira ya biashara husika, wenye kuelezea vizuri tahadhari zinazohusiana na biashara husika, wenye kubainisha vizuri vielelezo zinavyoonesha uwezekano wa kufanyika biashara husika, na wenye mambo ya kuvutia kivitendo na yenye kuwasisimua/kuvutia wawekezaji
Mpango wa biashara una faida mbalimbali kwa biashara husika na kwa mwenye biashara. Baadhi ya faida za mpango wa biashara ni kama ifuatavyo: unaonyesha tathimini ya uchunguzi wa uwezekano au uhalisia wa wazo jipya la biashara kimalengo na kiuchambuzi pasipo kutawaliwa na hisia za mtu binafsi kwa kuonyesha uwepo wa masoko na kiasi kinachotarajiwa kuuzwa katika masoko husika, uwezo wa menejimenti katika kuendesha biashara, na kama biashara inaweza kujiendesha kwa faida.
Mpango wa biashara unadokeza namna ya kuendesha biashara kwa mafanikio zaidi kwa kubainisha fursa na kuepukana na makosa, kuendeleza uzalishaji, usimamizi na mipango ya masoko, kutengeza bajeti na makadirio ya upatikanaji wa fedha.
Mpango wa biashara unanadi au unelezea wazo la biashara kwa watu wengine na hivyo kutumika kama msingi wa fedha mradi kwa kubaini kiasi na aina ya mtaji unaohitajika, kukadiria faida na marejesho ya uwekezaji, na kubashiri uingia wa pesa taslimu, uwezo wa kulipia huduma na hulipaji deni.
Mjasiriamali mdogo anatakiwa kutambua kuwa mpango mzuri wa biashara na utekelezaji wa mpango huo ndiyo njia pekee inayoweza kusaidia biashara yake
 Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa