TAWCA YAPONGEZWA KWA KUWA NGUZO YA UCHUMI WA KIDIJITALI, UADILIFU

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), akizungumza wakati akifungua Mkutano wa Tisa wa Chama cha Wanawake Wahasibu -TAWCA wenye kaulimbiu “Uongozi unaozingatia kuacha alama katika enzi ya kidijitali: Ubunifu wenye uadilifu kwa matokeo endelevu”, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), katika hoteli ya Malaika Resort, jijini Mwanza, ambapo alikipongeza chama hicho kwa mchango wake katika tasnia ya uhasibu nchini lakini pia kwa kuimarika na kuwa taasisi muhimu katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi nchini.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (wa pili kulia), akimkabidhi Tuzo Mwakilishi wa Kampuni ya EY, Bi, Neema Kiure (wa pili kushoto), kwa kutambua mchango wao katika kufanikisha Mkutano wa Tisa wa Chama cha Wanawake Wahasibu, uliofanyika katika hoteli ya Malaika Resort, jijini Mwanza. Wengine katika picha ni Mwenyekiti wa Chama cha Wahasibu (TAWCA), CPA Mary Mabiti, (kushoto) na Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho, CPA. Anna Mzinga (kulia).
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (wa pili kulia), akimkabidhi Tuzo Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Mzenzi (wa pili kushoto), kwa kutambua mchango wao katika kufanikisha Mkutano wa Tisa wa Chama cha Wanawake Wahasibu, uliofanyika katika hoteli ya Malaika Resort, jijini Mwanza. Wengine katika picha ni Mwenyekiti wa Chama cha Wahasibu Wahasibu (TAWCA), CPA Mary Mabiti, (kushoto) na Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho, CPA. Anna Mzinga (kulia).

Baadhi ya Wanachama wa Chama cha Wanawake Wahasibu -TAWCA wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (hayupo pichani), wakati akifungua Mkutano wa Tisa wa Chama hicho wenye kaulimbiu “Uongozi unaozingatia kuacha alama katika enzi ya kidijitali: Ubunifu wenye uadilifu kwa matokeo endelevu”, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), katika hoteli ya Malaika Resort, jijini Mwanza, ambapo alikipongeza chama hicho kwa mchango wake katika tasnia ya uhasibu nchini lakini pia kwa kuimarika na kuwa taasisi muhimu katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi nchini.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (katikati), akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Chama cha Wahasibu Wahasibu (TAWCA), CPA Mary Mabiti, (kushoto) na Mkurugenzi Mtendaji wa Chama hicho aliyemaliza muda wake, CPA. Tumaini Lawrence, mara baada ya kufungua Mkutano wa Tisa wa Chama hicho wenye kaulimbiu “Uongozi unaozingatia kuacha alama katika enzi ya kidijitali: Ubunifu wenye uadilifu kwa matokeo endelevu”, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), katika hoteli ya Malaika Resort, jijini Mwanza, ambapo alikipongeza chama hicho kwa mchango wake katika tasnia ya uhasibu nchini lakini pia kwa kuimarika na kuwa taasisi muhimu katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi nchini.

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb) (Katikati aliyeketi), Mhasibu Mkuu wa Serikali, CPA Leonard Mkude (wa pili kushoto aliyeketi), Mwenyekiti wa Chama cha Wahasibu (TAWCA), CPA Mary Mabiti, (wa pili kulia), Mkurugenzi Mtendaji wa TAWCA, CPA. Erica Kiduko (kushoto aliyeketi), na Mlezi wa Chama hicho ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Mzenzi (kulia aliyeketi), wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wanachama wa TAWCA kutoka Wizara ya Fedha,  wakati wa hafla ya kufungua Mkutano wa Tisa wa Chama hicho wenye kaulimbiu “Uongozi unaozingatia kuacha alama katika enzi ya kidijitali: Ubunifu wenye uadilifu kwa matokeo endelevu” iliyofanyika katika hoteli ya Malaika Resort, jijini Mwanza.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Mwanza) a

Msaada wenu tafadhali

Na. Joseph Mahumi, WF, Mwanza

Serikali imekipongeza Chama cha Wanawake Wahasibu Tanzania (TAWCA), kwa mchango wake katika tasnia ya uhasibu nchini lakini pia kwa kuimarika na kuwa taasisi muhimu katika kuchochea maendeleo ya kiuchumi nchini.

Pongezi hizo zimetolewa na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), wakati akifungua Mkutano wa Tisa wa Chama cha Wanawake Wahasibu -TAWCA wenye kaulimbiu “Uongozi unaozingatia kuacha alama katika enzi ya kidijitali: Ubunifu wenye uadilifu kwa matokeo endelevu”, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), katika hoteli ya Malaika Resort, jijini Mwanza.

Mhe. Munde alisema kuwa, maendeleo ya chama hicho kutoka kundi la waanzilishi 18 hadi kuwa na zaidi ya wanachama hai 1,200 ni ishara ya uwezo wa wanawake wataalamu katika kujenga taasisi imara na kuchangia maendeleo ya taifa.

Alisema TAWCA imevuka mipaka ya kuwa chama cha kitaaluma pekee na sasa imekuwa sehemu muhimu ya juhudi za kujenga uwezo wa kiuchumi, kukuza rasilimali watu na kuimarisha usimamizi wa fedha nchini.

“Jitihada mbalimbali zinazofanywa na TAWCA katika kuwawezesha wanawake kiuchumi, ni dhahiri kuwa unaendana na juhudi za Serikali za kuimarisha matumizi ya teknolojia katika usimamizi wa fedha za umma, kuongeza uwazi na kudhibiti upotevu wa rasilimali, na zinaunga mkono azma ya Serikali kufikia ujumuishaji wa kiuchumi unaowanufaisha wananchi kuanzia ngazi ya chini” aliseme Mhe. Munde

Mhe. Munde alisema kuwa kupitia mpango wa “Bado Naweza”, wa TAWCA imewajengea uwezo wa kibiashara wanawake vijana 101, kutoa mwongozo kwa wafanyabiashara wanawake 208, kufanikisha kiwango cha urejeshaji wa mikopo kufikia asilimia 96, kuongeza mfuko wa TAWCA SACCOS hadi zaidi ya Shilingi milioni 520, hatua ambayo inasaidia kujenga uwezo wa wanachama na kuongeza mtaji wa ndani.

“Kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Serikali kwa ujumla, ninaahidi kuendelea kuiunga mkono TAWCA na kutoa wito kwa Wizara, taasisi za Serikali, washirika wa maendeleo, wafanyabiashara na wadhamini kushirikiana na chama hicho katika kutekeleza programu zake” alisema Mhe. Munde

Mhe. Munde aliwataka washiriki wa mkutano huo kutumia jukwaa hilo kujadili mawazo mapya na ya kijasiri katika masuala ya fedha, kuimarisha ushauri kati ya vizazi na kuweka hatua madhubuti za kuendeleza taaluma ya uhasibu kwa kuzingatia viwango vya juu vya uadilifu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Wahasibu (TAWCA), CPA Mary Mabiti, alieleza kuwa safari ya chama hicho imejengwa katika misingi ya ushirikiano, uwezeshaji na kujenga uwezo wa wanawake katika taaluma ya uhasibu.

Alisema tangu kuanzishwa kwake mwaka 2015, TAWCA imeendelea kuwa jukwaa muhimu la kuwaunganisha wanawake wataalamu wa uhasibu, kuwawezesha vijana kupitia mafunzo, programu za mafunzo kwa vitendo na maendeleo ya taaluma, huku ikisisitiza umuhimu wa kujifunza kwa kuendelea, ubunifu na kuendana na mabadiliko ya mazingira ya biashara ya kimataifa.

“Mafanikio yaliyofikiwa yamechangiwa na ushirikiano kati ya TAWCA, Serikali, Bodi ya Uhasibu Tanzania -NBAA, taasisi mbalimbali, washirika na wadau, nguvu ya pamoja ni muhimu katika kuendeleza taaluma, kuwawezesha wanawake na kuchangia maendeleo ya Taifa” alisema Bi. Mabiti

Naye Mlezi wa TAWCA ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA), CPA Prof. Siasa Mzenzi, amekihakikishia Chama hicho ushirikiano na msaada wa Serikali katika kuendeleza na kutekeleza mipango yake ya kukuza taaluma ya uhasibu nchini.

CPA. Prof. Mzenzi aliitaka TAWCA kujifunza kutoka kwa taasisi na jumuiya za kitaaluma zinazofanya vizuri barani Afrika, huku Tanzania ikitumia fursa hiyo kubadilishana uzoefu na mbinu bora katika kuimarisha taasisi hiyo na kujenga jumuiya ya wataalamu wa uhasibu iliyo imara, jumuishi na yenye mchango mkubwa katika maendeleo ya Taifa.





Mhe. Deus Sangu Ashiriki Shughuli za Uvuvi Kirumba Katika Muendelezo wa Utoaji Elimu ya Skimu ya Hifadhi


*Mkurugenzi Mkuu wa NSSF Aeleza Mafao na Faida za Skimu ya Hifadhi

Na MWANDISHI WETU,
Mwanza. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu, ameongoza utoaji wa elimu ya hifadhi ya jamii kwa wananchi waliojiajiri Kanda ya Ziwa, huku akiwahamasisha kujiwekea akiba kwa ajili ya maisha yao ya sasa na baadaye.

Alisema hayo wakati wa muendelezo wa utoaji wa elimu ya Skimu ya Hifadhi uliofanyika katika Soko la Kimataifa la Samaki Kirumba jijini Mwanza, tarehe 6 Machi 2026.

Katika ziara hiyo ya kikazi, Waziri Sangu aliangalia shughuli za wajasiriamali wakiwemo wavuvi na kushiriki kuvua samaki pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba.

Ziara hiyo imemsaidia kuelewa mazingira ya kazi ya wananchi wanaolengwa na skimu hiyo.

Aliwataka wananchi wa Mwanza na mikoa jirani kujiunga na NSSF ili kujiwekea akiba na kunufaika na mafao yanayotolewa na Mfuko wa Taifa wa Hifadhi ya Jamii (NSSF).

Waziri Sangu alimshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuhakikisha wajasiriamali wanakuwa sehemu ya hifadhi ya jamii na kueleza kuwa skimu hiyo itasaidia Watanzania kuondokana na umasikini.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, alisema mkoa umejipanga kuandikisha wanachama wengi zaidi iwapo hamasa kubwa itaendelea.

“Sekta ya waliojiajiri imeimarika sana; wananchi wengi wanajihusisha na uvuvi, kilimo na shughuli nyingine za kipato. Kwa hamasa kama hii, tutawaandikisha wengi zaidi na kunufaika na mafao yanayotolewa na NSSF,” alisema.

Naye, Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba aliwataka waliojiajiri kujiunga na kuchangia skimu hiyo, ambapo wananufaika na mafao mbalimbali ikiwemo pensheni ya uzee, urithi, ulemavu, matibabu na huduma nyingine.

Alibainisha kuwa mfumo wa uchangiaji ni rafiki, ukiwa na kiwango cha chini cha shilingi 30,000 au 52,200 kwa mwezi, kinachowawezesha wanachama na familia zao kunufaika.

Awali, Mbunge wa Ilemela, Mhe. Kafiti Kafiti, aliipongeza Serikali ya Awamu ya Sita kwa kuwajumuisha wananchi waliojiajiri kunufaika na hifadhi ya jamii kama wanavyonufaika wafanyakazi wa sekta binafsi na sekta ya umma.

“Ndugu zangu, kupata pensheni sio lazima uwe mtumishi wa Serikali au sekta binafsi. Yeyote anayejipatia kipato sasa ana fursa hiyo.
Milango imefunguliwa, na mimi kama balozi wa bodaboda na bajaji tunaendelea kufungua fursa ili watu wajiajiri, wachangie na kujiwekea akiba ya baadaye kupitia Mfuko wa NSSF,” alisema Mhe. Kafiti. 

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu akijionea shughuli za uvuvi katika maeneo ya kazi ya wavuvi katika Soko la Kimataifa la Samaki Kirumba jijini Mwanza, ambapo pia alishiriki kuvua samaki akishirikiana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa NSSF, Bw. Masha Mshomba.
 










 

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa