Tone

Tone

NAIBU WAZIRI MAVUNDE AAGIZA WAKURUGENZI KUPANDISHWA KIZIMBANI JIJINI MWANZA, NI KWA KUTOJISAJILI NA WCF

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.



NA K-VIS BLOG/Khalfan Said, Mwanza

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Ajira na Vijana, Mhe. Antony Mavunde, (pichani juu), ameagiza waajiri ambao hawajajisajili na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi kufanya hivyo, vinginevyo wafikishwe mahakamani mara moja.

 Mhe. Mavunde ametoa agizo hilo Jumatatu Februari 26, 2018 baada ya kufanya ziara ya kushtukiza jijini Mwanza, kubaini waajiri ambao bado hawajatekeelza takwa la kisheria kifungu cha 5 cha Sheria ya Fidia Kwa Wafanyakazi, Sura 263 marejeo ya mwaka 2015, ambayo inamtaka kila mwajiri kutoka sekta ya umma na binafsi Tanzania bara awe amejisajili na kuwasilisha michango kwenye Mfuko huo.



Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko huo, Bw. Anslem Peter,  jiji la Mwanza pekee lina waajiri 1228, lakini kati ya hao ni waajiri 482 tu ndio waliojisajili na Mfuko huku waajiri wengine 746 wakiwa bado hawajajisajili. Hali hiyo ndiyo iliyomfanya Mhe. Naibu Waziri kufanya ziara hiyo ya ghafla.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari mara baada ya ukaguzi huo wa kushtukiza, Mhe. Mavunde pia ameiagiza WCF kuwafikisha mahakamani mara moja, waajiri wa kampuni ya ujenzi ya JASCO, (Mkurugenzi Mtendaji Bw.Karan Bachu),

Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Airco Holdings  inayotoa huduma za kusogeza vifurushi na mizigo uwanja wa ndege wa Mwanza na hoteli ya Belmonte ya jijini humo ambapo Mkurugenzi Mtendaji wa Hoteli hiyo, Bw. Philemon Tei, amejikuta matatani.

"Naagiza  waajiri hao kulipa michango yote ya nyuma (tangu tarehe 1 Julai 2015 tangu Mfuko ulipoanza kutekeelza majukumu yake au siku mwajiri aliyoanza kazi zake iwapo ni baada ya tarehe 1 Julai 2015).

Mhe. Mavunde ameagiza waajiri hao kufanya mawasiliano na watendaji wa Mfuko haraka iwezekanavyo ili kuweza kubaini kiwango cha riba kila mwajiri anachopaswa kulipa kutokana na kuchelewesha michango katika Mfuko. “Ni kosa la jinai kwa mwajiri kutotekelza takwa hilo la kisheria na kifungu cha 71(4) cha Sheria ya Fidia kwa Wafanyakazi kimeweka wazi kuwa mwajiri wa aina hii, anaweza kutozwa faini isiyozidi shilingi milioni 50,000, kifungo kisichozidi miaka 5 jela au adhabu zote kwa pamoja, kwa hivyo nitoe wito kwa waajiri hao, hakuna sababu ya kushurutishwa kutekeleza sheria.
"Tutatekelza agizo la Mhe. Waziri kama alivyolitoa, na nitoe rai tu kwa waajiri kote nchini (Tanzania Bara), kutekeleza takwa hilo la kisheria, kwani hakuna kichaka cha kujificha tutawafikia." Alisisitiza Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko huo, Bw. Anslem Peter katika taarifa yake kwa waandishi wa habari.

NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Ajira na Vijana, Mhe. Antony Mavunde(kushoto), akiwa na Mkurugenzi wa Uendeshaji wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, 9WCF), Bw. Anslem Peter,  akitoa maagizo ya kufikishwa mahakamani mara moja mkurugenzi mtendaji wa Belmonte Hotel ya jijini Mwanza leo Februari 26, 2018 kwa kushindwa kutekeleza takwa la kisheria linalomtaka kujisajili na Mfuko huo. Naibu waziri ameonya waajiri wote nchini kuttekeleza wajibu wao kwani hakuna mahala pa kujificha na operesheni hiyo inaendelea mikoa mingine.
 
 NAIBU Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, anayeshughulikia Kazi, Ajira na Vijana, Mhe. Antony Mavunde, (wakwanza kushoto), Mkurugenzi wa Uenmdeshaji (Director of Operations), Anslem Peter,  Afisa Kazi Mfawidi Mkoa wa Mwanza, Khadija Hersi, wakipitia nyaraka za Hoteli ya Belmonte ya jijini Mwanza kuona jinsi uongozi wa hoteli hiyo unavyotekeleza Sheria ya Fidia Kwa wafanyakazi, kwa kujisajili na Mfuko huo. Naibu Waziri alifanya ziara ya kushtuikiza kwenye kampuni kadhaa jijini Mwanza ambapo hoteli hiyo ilibainika kutojisajili na aliamuru Mkurugenzi wake kupelekewa mahakamani mara moja. Wakwanza kulia aliyesimama ni Mkuu wa KItengo cha Mawasiliano na Uhusiano WCF, Bi. Laura Kunenge.
 Naibu waziri akiongozana na Bw. Anslem Peter na afisa mwingine kutoka jijini Mwanza mara baada ya kukagua ofisi za huduma za vifuriushi na mizigo uwanja wa ndege wa Mwanza, Airco Holdings.
Mkurugenzi wa Belmonet Hotel ya jijini Mwanza, Bw.Philemon Tei
Naibu Waziri Mvunde, akizungumza na wafanyakazi wa Airco Holdings ya uwanja wa ndege wa Mwanza. Kushoto ni Bw. Anslem Peter

 Naibu Waziri akiwa kwenye ofisi za Airco Holdings uwanja wa ndege wa jijini Mwanza
 Naibu Waziri akitoa maelekezo kwa uongozi wa Belmonte Hotel



 Maafisa wa WCF, wakiongozwa na Mkurugenzi wa Uendeshaji, Bw. Anslem Peter, (kushoto) na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano, Bi. Laura Kunenge, wakitoka kwenye kiwanda cha kuchakata samaki jijini humo baada ya ukaguzi huo wa kushtukiza.
 Mkurugenzi wa kampuni ya ujenzi ya JASCO, ya jijini Mwanza Bw. Karan Bachu, akijieleza mbele ya Naibu Waziri Mvunde, (hayupo pichani)
 Mhe. Mavunde, (kushoto), akizungumza mbele ya Mkurugenzi wa kampuni ya ujenzi ya JASCO, ya jijini Mwanza Bw. Karan Bachu
 Mhe. Mavunde, akizungumza na wafanyakazi wa kampuni ya ujenzi ya JASCO ya jijini Mwanza baada ya kufanya ukaguzi wa kushtukiza leo Februari 26, 2018.
 Mhe. Mavunde na maafisa wa WCF wakiwa ofisi za kampuni ya kuchataka samaki jijini Mwnaza
 Mhe. Naibu Waziri akipitia nayaraka za kampuni ya kuchakata samaki ya jijini Mwnaza wakati wa ukaguzi wake.
Mkurugenzi wa Uendeshaji wa WCF, Bw. Anslem Peter akimuonyesha nyaraka za kampuni ya uchakataji samaki jijini Mwanza, ambayo imeanza kuwasilisha michango, lakini bado haijajisajili na Mfuko, ambapo aliagiza watekeeleze takwa hilo haraka.

TAMASHA LA PASAKA 2018 KUMNG'ARISHA ROSE MUHANDO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam wakati akielezea maandalizi kabambe ya Tamasha la pasaka linalotarajia kufanyika Aprili mosi katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na baadae tamasha hilo April 2, 2018 tamasha hilo litafanyika katika uwanja wa Halmashauri ndani ya Bariadi mkoani Simiyu.
Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dar es Salaam wakati akielezea maandalizi kabambe ya  Tamasha la  pasaka linalotarajia kufanyika Aprili mosi katika uwanja wa CCM Kirumba  jijini Mwanza na baadae tamasha hilo April 2,2018 tamasha hilo  litafanyika katika uwanja wa Halmashauri ndani ya Bariadi mkoani Simiyu.

Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG. 

Mwimbaji Mahiri wa nyimbo za Kiroho (Injili) Rose Muhando anatarajia kuizindua albamu yake ndani ya Tamasha la Pasaka linalotarajiwa kufanyika kufanyika Aprili mosi katika uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza na  baadae tamasha hilo April 2,2018 litafanyika katika uwanja 
wa Halmashauri ndani ya Bariadi mkoani Simiyu .

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Msama Promotion, Alex Msama ambao ndiyo waandaaji wa tamasha hilo, amesema maandalizi ya tamasha hilo yanaendelea vizuri na wanatarajia kuanzia katika jiji La Mwanza ndani ya Uwanja wa CCM-Kiruma Aprili 1, 2018 na kuelekea uwanja wa Halmashauri mjini Simiyu.

"Kwa kipindi kirefu Mwimbaji Rose Muhando amekuwa kimya kwa muda mrefu ila kwasasa namtangaza Kinara Rose Muhando ndiyo atakayeongoza jahazi la Tamasha la Pasaka kwa Mwaka 2018 hivyo wananchi mjitokeze kwa Wingi," amesema Msama. 

Aliongeza kuwa mbali na uzinduzi huo, tukio lingine kubwa litakalofanyika ni kuombea nchi amani,hukua kauli mbiu itakuwa "Upendo na Amani"

"Nipende kuwaomba wananchi wajitokeze kwa wingi katika tamasha la Pasaka ambalo litakuwa la namna yake na waje wajionee vipaji lukuki kutoka ndani ya Tanzania na nje. 


MAJALIWA ATEMBELEA SHULE YA MSINGI YA MITINDO INAYOLEA NA KUSOMESHA WATOTO WENYE UALBINO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na watoto wakati alipotembelea shule  ya msingi ya Mitindo wilayani Misungwi  na kufungua bweni la wavulana katika shule hiyo ambayo pia inalea  na kusomesha watoto wenye ulemavu wa ngozi , Februari 19, 2018. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe wakati alipofungua bweni la wavulana katika shule ya msing ya Mitindo wilayani Misungwi, Februari 19, 2018.Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella na watatu kulia ni Mbunge wa Misungwi, Charles Kitwanga.
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikagua mdawati katika madarasa ya shule ya msingi ya Mitindo wilayani Misungwi baada ya kufungua bweni la wavulana shuleni hapo Februari 19, 2018. Kushoto ni Mwalimu Mkuu wa Shule hyo, S. Mafie.
Wazri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na mtoto Januari  wa Shule ya Msingi ya Mitindo wilayani Misungwi ambayo pia inawalea na kuwasomesha watoto wenye ulemavu wa ngozi , Februari 19, 2018. Mtoto huyo siku zote amesisitiza kwamba baada ya kumaliza masomo yake akiwa mtu mzima angependa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania .
 Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa kwenye picha ya pamoja na  watoto alipotembelea Shule ya Msingi ya Mitindo ambayo pia inalea na kuwasomesha watoto  wenye ulemavu wa ngozi wilayani Misungwi Februari 19, 2018. Mheshimiwa Majaliwa pia alifungua bweni la wavulana shuleni hapo. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

NEC YARIDHISHWA NA MAANDALIZI YA VITUO 46 VYA KUPIGIA KURA KATA YA ISAMILO -MWANZA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

WATENDAJI TENGENI MUDA WA KUWAHUDUMIA WANANCHI-MAJALIWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwapungia wananchi wa Buchosa wakati alipoingia kwenye uwanja wa michezo wa Nyehunge wilayani Sengerema kuhutubia mkutano wa hadhara Februari 15, 2018.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa mmiliki wa kiwanda kidogo cha Dotto Posho Mill, Bw. Alexander Dotto (kushoto) kuhusu unga na Mchele unaozalishwa na kiwanda hicho kilichopo eneo la Bukara, Sengerema Februari 15, 2018. Kulia ni Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Miongella.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwasalimia wananchi wa Sengerema baada ya kuweka jiwe la msingi la kiwanda kidogo cha kusaga nafaka na kukoboa mpunga cha Dotto Posho Mill kilichopo eneo la Bukara, Sengerema Februari 15, 2018.Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka watendaji na wakuu wa idara mbalimbali kuhakikisha wanatenga muda na kwenda vijijini kuwahudumia wananchi.Amesema wananchi hususani waishio maeneo ya vijijini wanachangamoto mbalimbali ambazo zinatakiwa kupatiwa ufumbuzi na watendaji hao.

Aliyasema hayo jana (Alhamisi, Februari 15, 2018) alipozungumza kwa nyakati tofauti na watumishi na wananchi katika kata ya Nyehunge na Ibisabageni wilayani Sengerema akiwa katika ziara ya mkoa wa Mwanza.
Alisema Serikali imedhamiria kwa dhati kuwatumikia kwa lengo la kuwaondolea kero mbalimbali zinazowakabili, hivyo hakuna sababu ya watendaji kukaa maofisini.“Watumishi wanawajibu wa kuwafuata wananchi katika maeneo yao hasa vijijini kwa sababu si kila mwananchi anauwezo wa kufuata huduma katika ofisi zenu na atakayeshindwa kufanya hivyo hatutomvumilia.”
Waziri Mkuu aliongeza kuwa Serikali inawawezesha watumishi wake kwa kuwapatia vitendea kazi kama usafiri ili waweze kuwahudumia wananchi ipasavyo.Alisema kwa sababu ya kutotekeleza wajibu wao ipasavyo kumekuwa na kero na malalamiko mengi kutoka kwa wananchi na hivyo kusababisha wananchi kuwasilisha kero na malalamiko hayo wakati wa ziara za viongozi wakuu.
Katika hatua nyingine Waziri Mkuu aliwataka wananchi wanaofanya kazi katika kiwanda cha kuongeza thamani ya mazao ya nafaka cha Doto Alex Posho Meel kuwa waaminifu.Waziri Mkuu alisema wafanyakazi hao wanatakiwa wawe waaminifu na wafanye kazi kwa bidii ili kukiwezesha kiwanda hicho kuendelea na uzalishaji.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,
ALHAMISI, FEBRUARI 16, 201

MAHUSIANO YA KIMAPENZI BILA KUPIMA AFYA YADAIWA KUWA CHANZO KIKUBWA CHA MAAMBUKIZI YA VVU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Imeelezwa kuwa watu wengi wanaendelea kupata maambukizi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) kutokana na kuanza mahusiano ya kimapenzi bila kutambua afya zao hali inayosababisha waanze kuishi kama mume na mke bila kujua hali zao za kiafya. 

AGPAHI YATOA MAFUNZO YA HUDUMA ZA KISAIKOLOJIA KWA WAHUDUMU WA VITUO VYA TIBA NA MATUNZO MWANZA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Mratibu wa Kudhibiti Ukimwi mkoa wa Mwanza Dk. Pius Masele.
***
Shirika la Ariel Glaser Pediatric AIDS Healthcare Initiative (AGPAHI) limeendesha mafunzo kuhusu msaada na huduma za kisaikolojia kwa wahudumu wa jamii wanaosaidia kazi katika vituo vya tiba na matunzo kwa watu wanaoishi na Maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi (VVU) vilivyopo katika halmashauri za wilaya mkoani Mwanza.

NYAVU HARAMU ZA BILIONI 2.6 ZATEKETEZWA JIJINI MWANZA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Shehena ya nyavu haramu za uvuvi zenye thamani ya shilingi bilioni 2.6 zilizokamatwa katika maghala mbalimbali jijini Mwanza leo na kikosi kazi maalumu kilichoundwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi , Luhaga Mpina kutokomeza uvuvi haramu kwenye operesheni maalum inayoendelea Kanda ya Ziwa Victoria iliyopewa jina la operesheni Sangara zikiteketezwa kwa moto,Picha na John Mapepele

Shehena ya nyavu haramu za uvuvi zenye thamani ya shilingi bilioni 2.6 zilizokamatwa katika maghala mbalimbali jijini Mwanza leo na kikosi kazi maalumu kilichoundwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi , Luhaga Mpina kutokomeza uvuvi haramu kwenye operesheni maalum inayoendelea Kanda ya Ziwa Victoria iliyopewa jina la operesheni Sangara zikiteketezwa kwa moto,Picha na John Mapepele
Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mary Tesha akishiriki kwenye zoezi la kuteketeza nyavu haramu za uvuvi zenye thamani ya shilingi bilioni 2.6 zilizokamatwa katika maghala mbalimbali jijini Mwanza leo na kikosi kazi maalumu kilichoundwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi , Luhaga Mpina kutokomeza uvuvi haramu kwenye operesheni maalum inayoendelea Kanda ya Ziwa Victoria iliyopewa jina la operesheni Sangara zikiteketezwa kwa moto kulia mwenye suti ni Katibu Mkuu wa Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Uvuvi, Dkt. Yohana Budeba akishuhudia,Picha na John Mapepele
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Uvuvi, Dkt. Yohana Budeba wa kwanza kulia aliyevaa suti akishirikiana na Mkuu wa wilaya ya Nyamagana,Mary Tesha zoezi la kuteketeza nyavu haramu za uvuvi zenye thamani ya shilingi bilioni 2.6 zilizokamatwa katika maghala mbalimbali jijini Mwanza leo na kikosi kazi maalumu kilichoundwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi , Luhaga Mpina kutokomeza uvuvi haramu kwenye operesheni maalum inayoendelea Kanda ya Ziwa Victoria iliyopewa jina la operesheni Sangara ,Picha na John Mapepele


Na John Mapepele, Mwanza.

Katibu Mkuu wa Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Uvuvi, Dkt. Yohana Budeba ametaifisha na kuteketeza zaidi ya tani mia mbili za shehena ya nyavu haramu za uvuvi zenye thamani ya shilingi bilioni 2.6 zilizokamatwa katika maghala mbalimbali jijini Mwanza leo na kikosi kazi maalumu kilichoundwa na Waziri wa Mifugo na Uvuvi , Luhaga Mpina kutokomeza uvuvi haramu kwenye operesheni maalum inayoendelea Kanda ya Ziwa Victoria iliyopewa jina la operesheni Sangara .

Mbali na kuteketeza zana hizo haramu, Serikali pia imekusanya zaidi ya shilingi bilioni tano kama sehemu ya adhabu kwa wavuvi na wafanyabiashara waliokutwa na zana haramu pamoja na makosa ya utoroshaji mwani, samaki na mazao yake nje ya nchi.

Akizungumza na mamia ya wavuvi wakati wa kuteketeza nyavu hizo leo, katika dampo la Buhongwa nje kidogo ya jiji la Mwanza, Dkt. Budeba amesema hatua hizo kali zinazochukuliwa na Serikali dhidi ya uvuvi haramu hazilengi kuwaonea wafanyabiashara au wavuvi wanyonge bali zimelenga kuwatengenezea maisha bora ya kizazi cha sasa na baadae ili kiweze kunufaika na rasilimali zilizoko ziwani.Aidha Dkt. Budeba amesisitiza kuwa kikosi hicho kitaendelea na operesheni hiyo bila kuchoka hadi hapo uvuvi haramu na utoroshaji wa mazao ya uvuvi utakapokwisha ndani ya ziwa hilo.

Pia aliwaonya wamiliki wa viwanda na wafanyabiashara wanaotengeneza na kuuza nyavu hizo ambapo amesema Serikali ikiwabaini itawachukulia hatua kali za kisheria ikiwa ni pamoja na kuwafutia leseni zote za biashara zao. Alisema rasilimali zilizopo ndani ya ziwa hili ni mali ya wananchi viongozi wamepewa dhamana ya kuongoza kazi ya ulinzi tu na endapo uvuvi haramu utakomeshwa wananchi ndiyo watakaonufaika.

Pamoja na kuteketeza nyavu hizo haramu, Dkt Budeba alieleza hali ya upatikanaji wa samaki aina ya sangara katika Ziwa Victoria ambapo alisema kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi Tanzania (TAFIRI) mwaka 2017 unaonesha kuwa samaki waliochini ya sentimita 50 ni asilimia 96.6 hivyo samaki hawa ni wachanga na hawarusiwi kuvuliwa ambapo samaki walio zaidi ya sentimita 85 ni asilimia 0.4 tu ambao ni wazazi na hawarusiwi kuvuliwa pia. Samaki wa sentimita 50 mpaka 85 ambao ndio wanafaa kuvuliwa ni asilimia 3 tu.

Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Uvuvi wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Fatma Sobo amesema Idara itaendelea kutumia Sheria ya Uvuvi namba 22 ya mwaka 2003 na Kanuni zake za mwaka 2009 pamoja na Sheria nyingine za Mazingira ili kudhibiti Uvuvi haramu nchini.

Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mary Tesha alisema Serikali ya Wilaya hiyo itaendelea kuunga mkono juhudi za kupambana na uvuvi haramu na kuwachukulia hatua stahiki kuwataka wananchi kuendelea kuwafichua wavuvi haramu ili kulinda rasimali hiyo muhimu waliyopewa na Mungu.

Kwa upande wao baadhi ya wavuvi walimuomba Dkt. Budeba kuwasiliana na Wizara ya Viwanda na Biashara, ili kuona namna ya kudhibiti nyavu zisizoruhusiwa ambazo zinatengenezwa viwandani na baadae kuuziwa wavuvi.

Hivi karibuni watendaji wakuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi kwa kushirikiana na kikosi kazi kilichoundwa na Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi wameweza kukamata nyavu haramu, meli za uvuvi kutoka nje ya nchi zinazovua bia kufuata taratibu na mazao ya uvuvi yanayotoroshwa nje ya nchi ikiwemo mwani na samaki yenye mabilioni ya fedha huku Waziri Mwenye dhamana ya sekta hiyo Luhaga Mpina kuahidi kuwa operesheni hizo zitakuwa za kudumu hadi uuvi haramu utakapokoma.

MPINA AAGIZA VIWANDA VYA SAMAKI KANDA YA ZIWA VICTORIA KUANZA KAZI IFIKAPO JULAI MWAKA HUU.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina(mwenye miwani ) akishirikiana na Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Vincent  Anney na Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Bi Anarozy Nyamubi kuteketeza nyavu haramu zilizokamatwa na kikosi kazi  maalum alichokiunda hivi karibuni katika wilaya ya Musoma kulia ni Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Maendeleo ya Uvuvi, Emanueli Bulayi akishuhudia tukio hilo leo.(Na John Mapepele)
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Joelson Mpina akiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Anarozy Nyamubi baada ya kuteketeza nyavu haramu katika Wilaya ya Butiama leo. (Na John Mapepele)
Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Vincent  Anney akimwaga mafuta kwenye nyavu haramu ili kuzichoma moto katika kijiji cha Bwai Kumusoma wilayani Musoma leo. (Na John Mapepele)
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Joelson Mpina akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Bwai Kumusoma wilayani Musoma leo ambapo alishiriki zoezi la kuchoma nyavu haramu zilizokamatwa na kikosi kazi  cha kudhibiti uvuvi haramu Kanda ya Ziwa Victoria  alichokiunda hivi karibuni, kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Vincent  Anney akisoma majina ya  Wavuvi Haramu (Na John Mapepele)

Asisitiza operesheni ya kutokomeza uvuvi haramu kanda ziwa ni  ya kudumu
Na John Mapepele, Mara
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ameagiza viwanda vinne vya kuchakata samaki na mazao yake vilivyofungwa  katika  Mikoa ya Mwanza na Mara kuanza kazi mara moja ifikapo Julai Mosi mwaka huu, ambapo amewataka wamiliki kupeleka mipango kazi ya namna ya kuvifufua  kabla ya  kufikia mwezi Machi mwaka  wizarani kwake.
 Alivitaja viwanda hivyo kuwa ni Tan Perch Limited na Supreme Perch Limited vilivyopo Mwanza na  Mara Fish Packers Limited na Prime Catch Limited  katika mkoa wa Mara.
Waziri Mpina alizungumza hayo jana wakati alipokuwa kwenye ziara ya kikazi mkoani Mara na Mwanza kukagua operesheni maalum ya kutokomeza uvuvi haramu kanda ya Ziwa Victoria inayofanywa na kikosi kazi maalum alichokiunda hivi karibuni.
“Mimi kama Waziri mwenye dhamana ya Sekta ya Uvuvi nchini niliyepa kulinda raslimali za uvuvi nitahakikisha kwamba  ulinzi wa raslimali hizi ni wa kudumu, na usio na mwisho hadi uvuvi haramu utakapoisha  hapa nchini” alisisitiza Mpina
Waziri Mpina alipata fursa ya kuzungumza na Mkuu wa Mkoa wa Mara na Kamati ya Ulinzi ya Mkoa huo, wananchi katika maeneo tofauti na hatimaye kushiriki katika zoezi la kuchoma nyavu haramu ambapo hadi sasa zaidi ya nyavu zenye thamani ya shilingi bilioni nne zimechomwa moto katika zoezi linaloendelea la kudhibiti uvuvi haramu mkoani Mara.
Kamanda anayeongoza kikosi cha kupambana na kudhibiti uvuvi haramu na utoroshaji wa mazao ya uvuvi Kanda ya Mara, Bakari Lulela alimweleza Waziri Mpina kuwa operesheni hiyo imefanyika katika Wilaya za Musoma, Butiama, Rorya na Bunda na kufanikiwa kukamata na kuteketeza zana haramu zenye thamani ya sh. bilioni 3.2 huku wavuvi na wafanyabiashara wa samaki na mazao yake waliokiuka sheria ya uvuvi wakitozwa faini ya sh. milioni 189.
Waziri Mpina aliziagiza mamlaka zinazohusika kuwachukulia hatua Maafisa Uvuvi wa  Kijiji cha Bwai Kumsoma waliotuhumiwa kushirikiana na wavuvi haramu kuondolewa mara moja katika kijiji hicho ili kupisha uchunguzi na ikithibitika wachukuliwe hatua kali kwa mujibu wa sheria.
Naye Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dk. Vincent Anney amesema kwamba hayuko tayari kuona Wilaya yake inaendelea kuishi na watumishi wanaojihusisha na uvuvi haramu  na kwamba sheria kali zitachukuliwa dhidi yao ikiwa ni pamoja na kuwaondoa katika wilaya hiyo.
Aidha Waziri Mpina ameiagiza Wizara yake kuandaa bei elekezi ya kununua samaki itakayowezesha kuondokana na tabia ya wenye viwanda kushusha hovyo bei pindi samaki wanapoongezeka na hivyo kuwadhulumu wavuvi kupata malipo stahili yanayotokana na kazi yao.
Waziri Mpina alisema Ziwa Victoria ni hazina na raslimali kubwa kwa Tanzania ambapo inaaminika kuwa  ni la kwanza kwa ukubwa katika bara la Afrika kwa kuwa na eneo la 68,000Km2  na la pili duniani.
Alisema  pamoja  na umuhimu wa ziwa hili katika kukuza uchumi na kuboresha maisha ya watanzania bado linakabiliwa na shughuli za uvuvi haramu uliokithiri ambapo tafiti zinaonyesha kwamba kama hakutakuwa na jitihada za haraka za kutokomeza uvuvi haramu, ziwa hilo hali halitakuwa  na raslimali za uvuvi ikiwa ni pamoja na samaki katika kipindi cha miaka miwili ijayo.
Alitaja uvuvi haramu unaofanywa kuwa  ni pamoja na kuvua katika maeneo yasiyoruhusiwa, kutumia valiyombo visivyosajiliwa, kuvua bila leseni,kutumia sumu, kutumia nyavu za utali na kuvua samaki wachanga ama wazazi wasioruhusiwa.
Uvuvi haramu mwingini nikuvua kwa kokoro na  nyavu zenye macho madogo chini ya kiwango kinachokubalika kisheria, katuli, kumbakumba na gizagiza ambapo alisema Serikali imedhamilia kutokomeza  uvuvi huo haramu.
Aidha alisema operesheni hiyo katika kanda ya Ziwa Victoria dhidi  ya uvuvi  haramu ni ya kudumu na inafanyika kwa kuzingatia Sheria ya Uvuvi Na.22 yaMwaka 2003 na Kanuni 58(1) ya Uvuvi ya Mwaka 2009 na Sheria ya Mazingira Na 20 ya Mwaka 2004 kifungu Na(1), 65(1)a pia Sheria ya Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu Na 29 ya Mwaka 1994 ili kudhibiti uvuvi haramu ulioshamiri kiasi cha kutoweka kwa raslimali ya samaki katika ziwa hilo kwa faida ya vizazi vya sasa na baadaye.
Waziri Mpina alisema Tanzania inamiliki 51% ya Ziwa hili ikifuatiwa na Uganda 43% na nchi ya Kenya inamiliki 6%. Ziwa hili ni moja ya maziwa yanayozalisha samaki kwa wingi duniani kwa makadirio ya takribani tani 1,000,000 kwa mwaka  ambapo asilimia 60 ya uzalishaji wa samaki wake unatoka Tanzania hivyo juhudi za pamoja za kutokomeza uvuvi haramu zinahitajika.

MKAZI WA JIJI LA MWANZA AJISHINDIA MILIONI 40 ZA TATUMZUKA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilemela,Khadija Nyembo akimkabidhi mfano wa hundi  mkazi wa Buswelu,Ilemela,jijini Mwanza, Gibson Gratian Erasms,aliyejishindia kitita cha shilingi milioni 40 kwenye mchezo wa kubahatisha wa TatuMzuka uliofanyika jumapili iliyopita (Jackpot ya Jumapili).
 Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Ilemela,Khadija Nyembo akiwa katika picha ya pamoja na Mkazi wa Buswelu,Ilemela,jijini Mwanza, Gibson Gratian Erasms,aliyejishindia kitita cha shilingi milioni 40 kwenye mchezo wa kubahatisha wa TatuMzuka uliofanyika jumapili iliyopita (Jackpot ya Jumapili),sambamba na baadhi ya viongozi wa Ofisi ya Wilaya na pamoja na ndugu wa mshindi huyo.

LUKUVI AWAPOZA WANANCHI WA KIGOTO, KABUHORO MWANZA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi akizungumza jambo amlipozuru kwenye eneo la Kigoto lenye mgogoro kati ya wananchi na polisi. 
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi akimfafanulia jambo Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi alipozuru eneo la Kigoto Ilemela ambalo lina mgogoro baina ya wananchi na jeshi la polisi. Kushoro wa kwanza ni Meya wa Manispaa ya Ilemela Renatus Mulunga, wa pili kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela.
Waziri wa  Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi akimuuliza Meneja majengo na Mkaguzi wa polisi, Daud Mwakalobo (kulia) kama eneo wanalotaka kujenga gati la boti na nyumba za askari polisi liko kwenye ramani. PICHA ZOTE NA BALTAZAR MASHAKA\
Na Baltazar Mashaka, Mwanza.

WANANCHI wanaomiliki nyumba 664 katika mitaa ya Kigoto na Kabuhoro katika Kata ya Kirumba Manispaa ya Ilemela jijini Mwanza wametakiwa kuwa na subira wakati serikali ikitafuta ufumbuzi wa mgogoro uliopo kati yao na Jeshi la Polisi.

Pia wamezuiwa kujenga nyumba zingine mpya kwenye maeneo ya mitaa yao na badala yake wawe walinzi na kuonya watakaothubutu kujenga hawatalipwa fidia ambapo awali walitakiwa kuondoka na kupisha eneo hilo baada ya kuandikiwa ilani ya siku saba na jeshi la polisi.

Akizungumza na wananchi hao Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alisema serikali imesikia kilio chao na hivyo amekuja chunguza mgogoro huo ili ifanye uamuzi wa kuutatua.

 Alisema serikali inataka kufahamu mahitaji ya wananchi na polisi na kuonya wananchi wanaoishi kwenye maeneo hayo wasithubutu kujenga (kuongeza) majengo mengine zaidi ya yaliyopo sasa na watakaokaidi hawatalipwa fidia.

“Nimekuja kuangalia mgogoro huu na kuchungumza jambo hili ili serikali ifanye uamuzi. Msidhani nina majibu, majibu yatatolewa ndani ya mwaka mmoja lakini msituhubutu kuongeza nyumba zingine zaidi, kuweni walinzi wa maeneo haya na tunataka muwe maeneo mzuri ili tuwarasimishie,”alisema Lukuvi.

Waziri huyo wa ardhi alisisitiza baada ya uchunguzi atamshauri vizuri Rais John Magufuli namna ya kumaliza mgogoro huo baina ya wananchi na taasisi hiyo ya serikali.

Lukuvi alieleza eneo la Kigoto ambalo Polisi inadai inataka kujenga Chuo cha Polisi wanamaji, nyumba za askari na  gati la boti na meli za doria zinaweza kujengwa popote lakini eneo hilo lazima lipangwe upya hata kama matumizi yakibadilishwa kwa kuwa haiwezekani watu waishi kwenye nyumba za ovyo ovyo.

“Miaka 70 hadi leo kwa nini ujenzi haukuzuiwa,hakuna viongozi hapa na kama mngewashirikisha wangewasaidia kuzuia.Je, upembuzi yakinifu ulifanyika kwenye eneo mnalotaka kujenga mdomo huo wa gati la boti za polisi?

Aidha akizungumza kwa niaba ya wenzao ,Ferdinand Mtundubalo alimweleza Waziri kuwa hawana tatizo na ujenzi wa gati la boti za polisi isipokuwa warasimishiwe makazi yao ili waondokanane na mgogoro huo.

Katika hatua nyingine Waziri Lukuvi aliwataka wataalamu wa wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela waainishe eneo la Uwanja wa Ndege wa Mwanza na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kikosi cha Ihale ili kila mmoja alinde eneo lake.

Pia alishauri eneo la Nyamwilolelwa litakalobaki baada ya kutengwa la uwanja wa ndege na JWTZ lipimwe wapewe wananchi wa eneo wapatao 1,961 na kuhusu barabara ya Mwanza –Igombe uamuzi wa Rais Magufuli ubaki ulivyo na uheshimiwe. 
 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa