Home » » RC MTANDA AHIMIZA WELEDI KWA WAKANDARASI WAZAWA MIRADI YA SERIKALI,AZITAKA TAASISI KUJENGA VIWANJA VYA MICHEZO

RC MTANDA AHIMIZA WELEDI KWA WAKANDARASI WAZAWA MIRADI YA SERIKALI,AZITAKA TAASISI KUJENGA VIWANJA VYA MICHEZO




Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda leo Agosti 5,2024 amefanya ziara fupi ya ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa Taasisi ya Teknolojia Dar-e-s Salaam Tawi la Mwanza unao gharimu shs bilioni 37 unatekelezwa na Mkandarasi mzawa Kampuni ya Comfix Engineering na kuhimiza weledi katika miradi ya Serikali.

Mkuu huyo wa Mkoa akiwa na mkurugenzi wa tawi hilo Dkt.Albert Mmari amejionea hatua ya umaliziaji wa majengo manne ya ufundishaji,Taaluma na hosteli za wanaume na wanawake pamoja na uwanja wa michezo wa siku nyingi wa tawi hilo na kutaka uboreshwe ili uje kuwa na tija zaidi.

"Nimefurahishwa na uwanja huu na hapa naomba nitoe msisitizo,Taasisi zote za Serikali na binafsi jengeni viwanja vya michezo nchi yetu ipo mbioni kuwa mwenyeji wa michuano ya AFCON 2027 na huenda CCM Kirumba ukatumika mtajiongezea vipato timu zikija kufanya mazoezi,"amesisitiza Mtanda.

Amesema katika michuano ya ligi kuu ya NBC timu mbalimbali zitafika kucheza na Pamba Jiji FC na wakati zinajiandaa na mechi zitahitaji viwanja vya mazoezi.

Akizungumza kampuni za watanzania kupewa miradi mikubwa ya Serikali,Mtanda amesema ni wajibu wao kutanguliza uaminifu na kuikamilisha kwa wakati hali ambayo itawajengea kuaminiwa na Serikali.

"Huu mradi wa miundombinu hii uliogharimu fedha nyingi ni mfano mzuri kwa mkandarasi huyu,kila jengo naambiwa linakamilika mwaka huu,endeleeni na weledi huu,"Mtanda

Kwa upande wake mkurugenzi wa tawi hilo Dkt.Albert Mmari amesema ujenzi huo una malengo makuu matatu kuongeza udahili,kuongeza programu ya elimu ya ufundi na ushirikiano wa kikanda.

"Mara baada ya mradi huu kukamilika utakuwa na tija kwa nchi za Afrika Mashariki na kati kwa watu kuja kupata utaalamu wa juu namna ya kuzalisha bidhaa za ngozi,"Dkt.Mmari

Ujenzi huo wa majengo ya kisasa ulioanza mwaka 2019 na utakamilika mwaka huu.

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa