Tone

Tone
Home » » UKEREWE YATUMIA MIL.451 KUBORESHA MAZINGIRA YA HUDUMA YA AFYA

UKEREWE YATUMIA MIL.451 KUBORESHA MAZINGIRA YA HUDUMA YA AFYA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

HALMASHAURI  ya  wilaya  ya  Ukerewe Mwanza  inaendelea  kubolesha mazingirana na  miundombinu  ya  huduma za  afya  ili  kuvutia  wataalamu lengo likiwa  kuboresha huduma  hiyo kwa jamii. 
Kaimu  mganga  mkuu wa  wilaya  hiyo Dr. Nyanda  Kombe  amesema hayo  jana  wakati  anazungumzia  miradi minne   inayondelea  kutekelezwa kwa gharama ya sh. Mil.  451.

Alisema   miradi inatekelezwa  kwa fedha za ruzuku  ya serikali kuu kupitia    mpango  wa maendeleo  ya afya  ya  msingi  [MMAM]  na  fedha nyingine  ikitokana na  mpango wa maendeleo [CGD].

Alibainisha  kuwa  katika mwaka  wa fedha  wa  uliopita  tayari  wamepokea  sehemu ya fedha ya  utekelezaji wa miradi  hiyo ambapo hivi sasa ipo katika hatua mbali mbali ya utekelezaji wake.

Miradi hiyo  ni pamoja na  jengo la  Kliniki  ya uzazi na mtoto inayojengwa kwa gharama  ya sh. Mil. 230 na   nyumba ya watumishi   yenye  makazi ya  familia mbili  inayojengwa  kwa  gharama ya  sh. Mil. 60.

Miradi  mingine  ni ujenzi  wa  nyumba  ya kufikiwa  watumishi  yenye uwezo wa kupokea  watu  sita  inayojengwa  kwa gharama  ya sh. Mil. 141 pamoja na  jengo la  kupumzikia   wagonjwa  wakati wanasubili  huduma linalojengwa kwa gharama  ya sh. Mil.20.
Akielezea  juudi  zaidi za halmashauri  ya wilaya hiyo  za kuboresha huduma  ya  afya  Dr. Kombe  alisema  katika mwaka  ujao wa fedha  pia wameomba  sh. Mil. 361.32 kwaajiri ya ujenzi wa  zahanati  tatu na kituo kimoja cha  afya.

Alisema   kati  ya fedha  hizo  sh. Mil. 161 zimeombwa  kwaajiri ya  kujenga zahanati katika visiwa vidogo  vya   Kulazu , Chibasi  huku  nyingine  ikitakiwa kujengwa katika kijiji cha  Masonga, wakati  huo sh. Mil. 200 zimembwa kujenga  kituo cha afya  cha  mji wa  Nansio.

Alisema  miradi hiyo ni muimu na kuongeza kuwa  mbali ya kuvutia  watumishi pia  inaweka mazingira mazuri  ya utoaji huduma  za tiba  hasa  huduma ya   uzazi na mtoto ambayo miundombinu yake kwa sasa ni finyu ikilinganisha na watu mil. 1.5 wanaopata huduma hiyo kwa mwaka.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa