Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
CHAMA cha Walimu (CWT)  wilayani Morogoro, kimewataka walimu wote wa
 shule za msingi na sekondari  wilayani humo kuzisoma mara kwa mara 
sheria za utumishi wa umma, kuzielewa na  kuzitumia ipasavyo kama ngao 
pekee katika wajibu wao kazini na pindi wanapodai  haki zao.
  Rai hiyo ilitolewa na  Katibu wa chama hicho wilaya, Adam Bayinga, 
mjini Mtamba, Tarafa ya Matombo  wakati akitambulisha kitengo ‘Ke’ 
‘Umamawamo’ ndani ya chama hicho na  kuhamasisha walimu kujitokeza 
kuwania nafasi mbalimbali za uongozi.
  “Kuna sheria na kanuni  zinazoongoza utumishi wa umma, mwalimu ana 
mamlaka mbili zinazoweza kumfukuza  kazi katika mifumo miwili yaani 
kuachishwa kazi na utumishi na bila  utumishi…na kuna hatua ambazo 
lazima zifuatwe," alisema Bayinga.
Chanzo;tanzania Daima 
0 comments:
Post a Comment