Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
ALIYEKUWA Waziri  Mkuu katika Serikali ya Awamu ya Tatu, Frederick 
Sumaye, amewashauri waliomo kwenye  ndoa kuvumiliana katika mambo 
mbalimbali ili kuepuka chuki inayoweza  kusababisha mauaji.
  Sumaye alisema  hayo juzi mjini Mwanza wakati wa uzinduzi wa kitabu 
‘Furahia Ndoa’  kilichoandikwa na wachungaji Zakayo na Carol Nzogere.
  Akizungumza  katika uzinduzi huo, Sumaye alisema kuwepo kwa mifarakano
 ndani ya ndoa  kunasababisha maambukizi ya magonjwa ya zinaa na ukimwi,
 kwa kuwa hutafuta  wapenzi nje ya ndoa ama kwa kutimiza haja ya mwili 
au kwa kukomoana.
  “Familia  kuvurugika na watoto kukosa mapenzi ya wazazi huhamia 
mitaani, uchumi wa  familia kuvurugika na watoto kukosa mahitaji muhimu 
ambayo ni elimu, afya na  kujifunza tabia mbaya,” alisema Sumaye.
Chanzo;Tanzania Daima 
0 comments:
Post a Comment