Home » » RC MTANDA AKUTANA NA UONGOZI WA MADEREVA WA SERIKALI ,AWAAHIDI MAZINGIRA BORA YA KAZI

RC MTANDA AKUTANA NA UONGOZI WA MADEREVA WA SERIKALI ,AWAAHIDI MAZINGIRA BORA YA KAZI

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Said Mtanda leo Agosti 2,2024 amekutana na uongozi wa madereva wa Serikali mkoani humo na kuwaahidi mazingira mazuri ya kazi hasa maslahi yao

Mazungumzo hayo mafupi yaliyofanyika Ofisini kwake Mkuu huyo wa mkoa amesema  kazi siku zote ili zifanikiwe ni lazima kuwepo na hali ya kutegemeana na siyo kubaguana.

"Mmefanya vizuri kunipa ulezi wa chama chenu ni eneo ambalo nitalitendea vizuri kwa uzoefu nilionao,nitahakkikusha magari yote yanafufuliwa na yaliyo hatua ya kuuzwa yafanyiwe hivyo,amesisitiza Mtanda

Amewataka madereva kuyatunza magari ya Serikali na kutosita kutoa ushauri wa kiufundi inapo bidi kwa wakubwa wao ili vyombo hivyo viendelee kudumu na kuepuka hasara kwa Serikali.

Aidha amezitaka Taasisi zote za Serikali pamoja na Halmashauri kuhakikisha zinawapa ruhusa madereva wao kuhudhuria mkutano wao mkuu utakaofanyika kuanzia Agosti 18 hadi 23 mwaka huu Jijini Arusha na kufunguliwa na Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa

Mwenyekiti wa chama cha madereva wa Serikali  mkoani Mwanza Enock Jeremia amemuhakikishia mkuu huyo wa mkoa kiyazingatia maelekezo yote aliyowapa.


 

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa