Home » » TABCO: Wanawake wamilikishwe mirathi

TABCO: Wanawake wamilikishwe mirathi

SHIRIKA linalojishughulisha na kutetea haki za wanawake na watoto jijini Mwanza la TABCO, limeitaka jamii nchini kuwathamini na kuwapa wanawake haki ya kumiliki mirathi ya wenzi wao.
Kauli hiyo ilitolewa hivi karibuni na Mkurugenzi wa Shirika hilo la TABCO, Irene Kyamba, alipozungumza katika semina ya mafunzo ya wajibu wa kumiliki mirathi wanawake, iliyofanyika ukumbi wa Kisomo jijini hapa.
Alisema baadhi ya wanawake wamekuwa wakinyanyasika na kukosa haki zao za kumiliki mirathi, pindi mwenzi wake anapofariki dunia, jambo ambalo halikubaliki.
Irene alisema shirika lake limejiwekea malengo ya kuhakikisha linaendelea kutoa elimu kwa jamii juu ya kuondoa mila potofu zinazomkandamiza mwanamke kuhusiana na umiliki wa mali zilizoachwa na mwenzi wake, hivyo ni vema jamii ikabadilika na kumpa haki mwanamke.
“TABCO tumejipanga vizuri kuielimisha jamii iondokane na dhana potofu na kandamizi kwa mwanamke juu ya umiliki wa mirathi. Tunahitaji kuona mwanamke anaheshimiwa na kupewa haki stahili ya umiliki wa mirathi.
“Kwa maana hiyo, TABCO hatutarudi nyuma katika juhudi hizi nzuri na bora kwa ustawi wa jamii na taifa letu. Watoto nao lazima waheshimiwe na kuthaminiwa,” alisema.
Mwezeshaji wa shirika hilo, Mercy Kaniki, aliisihi jamii kuhakikisha inamtambua mwanamke kama sehemu muhimu katika nguzo na maendeleo ya familia
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa