WANAFUNZI
2,990 waliochaguliwa kujiunga na elimu wa sekondari mwaka huu
katika wilaya ya Ukerewe , Mwanza hadi sasa awajulikani walipo
Afisa elimu wa sekondari wa wilaya hiyo Slivester Mlimi ameliambia baraza la madiwani jana kuwa wanafunzi waliojitokeza na kupokelewa shuleni ni 1,775 ambao ni sawa na asilimia 38 ya wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu.
Akielezea ukubwa wa tatizo hilo alisema mbali asilimia 62 ya wanafunzi waliochaguliwa kushindwa kujitokeza pia wanafunzi 815 waliotakiwa kuingia kidato cha tatu mwaka huu hadi sasa awajulikani walipo.
Alisema kati ya wanafunzi hao 315 hatima yao aijulikani baada ya matokeo ya mtiani wa taifa wa kuingia kidato cha tatu kuzuiliwa kwa kushindwa kulipa mchango wa sh. 20,000 kila mmoja, na wengine zaidi ya 500 hawakufanya mtiani huo.
Akizungumzia tatizo hilo mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo Mhamed Munga alisema tayari ameagiza wanafunzi wote waliochaguliwa kujinga kidato cha kwanza wapokelewe shuleni bila masharti.
Alisema wakati wazazi wanaendelea kutafuta ada na michango mingine ikiwemo sare za shule wanafunzi hao wanatakiwa kuwa shule wakiendelea na masomo ilimradi wamepewa vifaa vya darasani kama daftari na kalamu.
Naye mkuu wa wilaya hiyo Mery Tesha aliyeshutushwa na suala hilo ameagiza hatua za makusudi zichukuliwe halaka ikiwemo kuendesha msako wa nyumba kwa nyumba ili kuhakikisha wanafunzi wote wanakwenda shule.
Alimtaka mkurugenzi awaagize viongozi wa ngazi za vijiji na kata wapewe orodha ya majina ya wazazi wanaozuia na hata kushindwa kuripa ada ya watoto wao watafutwe na kufukishwa mahakani kwa hatua za kisheria.
Akizungumzia tatizo hilo lililoelezwa na baadhi ya madiwani kuwa ni aibu na fedhea kubwa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo Joseph Mkundi amewataka viongozi na watendaji katika ngazi zote kutimiza wajibu wao.
Alisema miongoni mwa mambo waliyokubaliana katika kiako hicho ni pamoja na hadi kufikia katikati ya mwezi huu viongozi wa ngazi za vijiji wawe tayari wameitisha vikao pamoja na mikutano ya adhala ikiwa ni mkakati wa kukabili tatizo hilo.
Afisa elimu wa sekondari wa wilaya hiyo Slivester Mlimi ameliambia baraza la madiwani jana kuwa wanafunzi waliojitokeza na kupokelewa shuleni ni 1,775 ambao ni sawa na asilimia 38 ya wanafunzi wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu.
Akielezea ukubwa wa tatizo hilo alisema mbali asilimia 62 ya wanafunzi waliochaguliwa kushindwa kujitokeza pia wanafunzi 815 waliotakiwa kuingia kidato cha tatu mwaka huu hadi sasa awajulikani walipo.
Alisema kati ya wanafunzi hao 315 hatima yao aijulikani baada ya matokeo ya mtiani wa taifa wa kuingia kidato cha tatu kuzuiliwa kwa kushindwa kulipa mchango wa sh. 20,000 kila mmoja, na wengine zaidi ya 500 hawakufanya mtiani huo.
Akizungumzia tatizo hilo mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya hiyo Mhamed Munga alisema tayari ameagiza wanafunzi wote waliochaguliwa kujinga kidato cha kwanza wapokelewe shuleni bila masharti.
Alisema wakati wazazi wanaendelea kutafuta ada na michango mingine ikiwemo sare za shule wanafunzi hao wanatakiwa kuwa shule wakiendelea na masomo ilimradi wamepewa vifaa vya darasani kama daftari na kalamu.
Naye mkuu wa wilaya hiyo Mery Tesha aliyeshutushwa na suala hilo ameagiza hatua za makusudi zichukuliwe halaka ikiwemo kuendesha msako wa nyumba kwa nyumba ili kuhakikisha wanafunzi wote wanakwenda shule.
Alimtaka mkurugenzi awaagize viongozi wa ngazi za vijiji na kata wapewe orodha ya majina ya wazazi wanaozuia na hata kushindwa kuripa ada ya watoto wao watafutwe na kufukishwa mahakani kwa hatua za kisheria.
Akizungumzia tatizo hilo lililoelezwa na baadhi ya madiwani kuwa ni aibu na fedhea kubwa mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya hiyo Joseph Mkundi amewataka viongozi na watendaji katika ngazi zote kutimiza wajibu wao.
Alisema miongoni mwa mambo waliyokubaliana katika kiako hicho ni pamoja na hadi kufikia katikati ya mwezi huu viongozi wa ngazi za vijiji wawe tayari wameitisha vikao pamoja na mikutano ya adhala ikiwa ni mkakati wa kukabili tatizo hilo.
0 comments:
Post a Comment