MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman
Mbowe, amenusurika kifo baada ya gari alilokuwa akisafiria kutoka
jijini Mwanza kwenda wilayani Ngara, Kagera kupata ajali.
Ajali hiyo ilitokea jana saa 6 mchana, umbali wa kilometa mbili
kutoka Kata ya Katoro, Geita na inadaiwa kuwa gari alilokuwa akitumia
limeharibika sehemu ya mbele.
Taarifa za uhakika kutoka eneo la tukio zimeeleza kwamba chanzo cha
ajali hiyo iliyosababishwa na mwendesha pikipiki yenye namba za usajili
T 212 BFR aliyefahamika kwa jina la Sayi Kahindi (32) mkulima,
mwenyeji wa Kijiji cha Inyala kuingia ghafla barabarani.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi
Rasmi ya Upinzani Bungeni wakati ajali hiyo ikitokea alikuwa akielekea
wilayani Ngara kwa ajili ya mikutano ya
Operesheni M4C Pamoja Daima iliyoanza hivi karibuni nchi nzima.
Operesheni M4C Pamoja Daima iliyoanza hivi karibuni nchi nzima.
Inadaiwa kwamba, Mbowe katika safari hiyo alikuwa akitumia gari la
Mbunge wa Ilemela, Highness Kiwia (CHADEMA) lenye namba za usajili T
217 CPB.
Baada ya ajali hiyo Mbowe ambaye pia ni Mbunge wa Hai, Kilimanjaro
alipata gari jingine lenye namba za usajili T 888 CGT Pajero, mali ya
mkazi wa Katoro, aliyejulikana kwa jina la Mbanju, ambalo lilimpeleka
Ngara anakoendelea na mikutano ya kukijenga chama wakati dereva na gari
lililopata ajali vikipelekwa kituo cha polisi.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Usalama Barabarani mkoani Geita, John Mfinanga
na Mkuu wa Polisi wa Wilaya ya Geita, Kamanda Bwire, walithibitisha
kuwepo kwa ajali hiyo na kuongeza kuwa uchunguzi wa chanzo cha ajali
unaendelea.
“Nimezungumza na mwenyekiti mwenyewe Mbowe ameniambia ni kweli
alipata ajali umbali wa kilometa mbili hivi kutoka mji wa Katoro
akielekea Chato.
“Gari alilokuwa akisafiria limeharibika vibaya maeneo ya mbele.
Pikipiki nayo imeharibika sana… wakati nawasiliana naye alikuwa
ameshaondoka eneo la tukio akielekea Bihalamuro kwenda Ngara,” alisema
Mbunge wa Nyamagana, Ezekiah Wenje.
Kesho Mbowe anatarajiwa kutua Geita kwa helikopta ili kuhutubia
mikutano ya hadhara katika mwendelezo wa shughuli za kukijenga chama
chake
Chanzo;Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment