Home » » Ewura yafungia kituo pekee cha mafuta

Ewura yafungia kituo pekee cha mafuta

Mafuta yakiwekwa katika gari, Ewura ipo kwenye operesheni ya kuvifungia vituo vya vinavyouza mafuta ambavyo havikidhi viwango vya ubora

Misungwi. Kituo cha kuuza mafuta wilayani Misungwi, mkoani Mwanza, kimefungwa na Mamlaka ya Udhibiti Nishati na Maji (Ewura) hadi kitakapokamilisha ujenzi wa paa.
Kwa mujibu wa barua ya Ewura ya Desemba 13 mwaka jana iliyosainiwa na Mkurugenzi Mkuu, Miriam Mahanyu inakitaka kituo hicho kufungwa hadi kikamilishe ujenzi
Mkurugenzi wa kituo hicho, Rashid Nassoro alisema alipokea barua hiyo Januari 24 mwaka huu.
Nassoro aliomba Ewura kumruhusu kuendelea na huduma, huku akiendelea kukamilisha ujenzi. “Kwa kuwa agizo hili limekuja tukiwa na akiba ya mafuta ya mwezi mmoja,” alisema.
Baadhi ya wakazi wamelalamikia hatua hiyo, kutokana na kuwa kituo pekee kinachotoa huduma.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa