Home » » Wataalamu maabara ya uvuvi waeleza changamoto zao

Wataalamu maabara ya uvuvi waeleza changamoto zao

WATAALAMU kutoka Maabara ya Taifa ya Kudhibiti Ubora wa Mazao ya Uvuvi, wamesema licha ya kuwa kufanikiwa bado, kuna changamoto zinazowakabili.
Hayo waliyazungumza jana mbele ya Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi, Dk. Titus Kamani, aliyetembelea maabara hiyo iliyopo mkoani hapa kujionea hali halisi ya utendaji.
Akielezea changamoto hizo, Ofisa Mfawidhi wa Kitengo cha Kudhibiti Ubora wa Mazao ya Samaki, Steven Lukanga, alizitaja kuwa ni tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara kiasi cha kuwalazimu kutumia jenereta na ukosefu wa wataalamu wa mitambo ya ukaguzi.
Kwa mujibu wa ofisa huyo, tangu kuanzisha kwa maabara hiyo mwaka 2003, hawakuwa wanatoza fedha zozote wafanyabiashara wa mazao ya uvuvi, lakini kwa sasa wanatoza kiasi cha sh 50,000 kuanzia tani 10.
Mkuu wa Idara  ya Kemikali, Longinus Tegulirwa, alisema mitambo iliyopo katika maabara hiyo ina uwezo mkubwa kwa kupima mazao mbalimbali licha ya kwamba wateja wa mazao hayo ni wachache.
Kwa upande wake, Dk. Kamani alisema amevutiwa na viwango vya vifaa na hali ya kuthibitisha ubora, na kwamba ni vema mazao ya samaki wa Tanzania yawe na ubora wa kutosha ili kuvutia soko la ndani na nje ya nchi.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa