Home » » BODI YA USHAURI YA TFDA KWA WIZARA YA AFYA YAKUTANA NA MKUU WA MKOA WA MWANZA

BODI YA USHAURI YA TFDA KWA WIZARA YA AFYA YAKUTANA NA MKUU WA MKOA WA MWANZA

Bodi ya  Ushauri ya Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) kwa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii (MAB) yakutana na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Injinia Evalist Ndikilo kwa lengo la kutambua mchango wa mkoa na ushirikiano unaotolewa kwa TFDA katika masuala ya Udhibiti wa Bidhaa za Chakula, Dawa, Vipodozi  na Vifaa tiba.

Akizungumza katika ziara hiyo Mwenyekiti wa MAB, Balozi Dkt. Ben Moses, amepongeza ushirikiano uliopo baina ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na TFDA kanda ya Ziwa na kutoa wito wa kudumisha ushirikiano uliopo kwa  kuwa lengo la udhibiti litafanikiwa ikiwa ushirikiano uliopo utadumishwa. 

'

Naye Mkuu wa Mkoa amesifu kazi kubwa inayofanywa na TFDA katika kulinda afya ya wananchi kwani afya za wananchi zikiimarika basi uchumi wa unchi nao utaimarika. Vilevile,  katika kueleza changamoto ambazo mkoa unakabiliana nazo katika masuala ya udhibiti wa chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba,  Injinia Ndikilo alieleza kuwa  usafi katika machinjio ni changamoto kubwa na kwamba anatarajia kulipatia ufumbuzi hivi karibuni baada ya kuitisha kikao cha wadau.

Aidha, Injinia Ndikilo ametoa wito kwa  TFDA  kuona fursa iliyopo ya kuhamasisha wafanya biashara kujenga kiwanda cha dawa jijini Mwanza kutokana na idadi kubwa ya wananchi pamoja na kuimarisha udhibiti wa bidhaa za chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba kufuatia kujengwa kwa kituo cha Biashara cha Jiji la mwanza ambapo milango ya biashara nyingi itakuwa wazi hususan bidhaa zinazodhibitiwa na TFDA.


Wajumbe wakiendelea na mazungumzo Yao na Mkuu wa mkoa wa Mwanza.
Mkuu wa mkoa wa Mwanza, Injinia Ndikilo, akifafanua jambo kwa wajumbe wa Bodi ya TFDA ofisini kwake.

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa