Watu 
 wawili wamefariki dunia papo hapo na wengine wanane kujeruhiwa vibaya 
katika ajali ya mabasi mawili yakugongana uso kwa uso katika kijiji cha 
Kamanga, Sengerema mkoani Mwanza saa nne asubuhi jana.
Akizungumzia
 ajali hiyo, shuhuda aliyekuwa katika pikipiki na kunusurika kugongwa na
 mabasi hayo, Philipo Budeba, alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo 
kasi wa mabasi yote mawili.
“Mimi
 nilikuwa naendesha pikipiki, mbele yangu kulikuwa na basi la Mkombozi 
Trans lenye namba T540 DLF na nyuma kulikuwa na Basi la Walawi Express 
lenye namba T167 CSN yote yalikuwa na mwendokasi," alisema Budeba.
"Dereva
 wa Mkombozi ndiye aliyetaka kupita gari lingine, lakini ilishindikana 
na kusababisha magari hayo kuvaana... mimi nilijirusha kwenye kilima cha
 pembeni mwa barabara."
Naye
 abiria wa Mkombozi Trans iliyokuwa ikitokea Kanyara Buchosa, Sengerema,
 Fransisco Kansola alisema tabia ya madereva kushindwa kuchukua 
tahadhari na kujali kuwahi abiria ndiyo chanzo cha ajali hiyo.
Walawi Express lilikuwa likitoka Mwanza kwenda Nemba wilayani Biharamulo.
Akithibitisha
 kutokea kwa ajali hiyo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi 
alisema dereva wa basi la Walawi, Frank Kimboka ni miongoni mwa majeruhi
 wanane wa ajali hiyo baada ya kujeruhiwa miguu yote.
“Waliofariki
 ni dereva wa basi la Mkombozi Trans aliyefahamika kwa jina la Simon 
Mdalesalamu na mwanamke aliyekadiriwa kuwa na umri wa miaka 18 hadi 20,"
 alisema Kamanda Msangi.
Majeruhi
 watatu wametajwa kuwa ni Frank Mushi aliyevunjika miguu yote miwili, 
Isaack Hamisi (22) mkazi wa Nyasaka wilayani Ilemela na Mwinyi Ismail 
(50) aliyevunjika miguu yote miwili, alisema Kamanda Msangi.
"Chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa mabasi hayo.”
Aidha,
 ajali hiyo ilitokea wakati mkoa wa Mwanza ukizindua maadhimisho ya wiki
 ya Nenda kwa Usalama Barabarani, yenye kaulimbiu inayosema ‘Zuia ajali,
 tii sheria, okoa maisha'.
Majeruhi walikimbizwa katika Hospitali ya Rufani ya Bugando jijini Mwanza kwa ajili ya matibabu.
 Kijukuu



0 comments:
Post a Comment