Tone

Tone
Home » » SERIKALI YADHAMIRIA KUFANIKISHA UTAFUTAJI NA UPATIKANAJI WA MAFUTA KATIKA BONDE LA EYASI WEMBERE NA ZIWA TANGANYIKA

SERIKALI YADHAMIRIA KUFANIKISHA UTAFUTAJI NA UPATIKANAJI WA MAFUTA KATIKA BONDE LA EYASI WEMBERE NA ZIWA TANGANYIKA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akiwa na Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa pamoja na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi na Naibu Waziri wa Nishati Dkt Medard Kalemani katika kikao na ujumbe wa wataalamu wa Sekta ya Nishati toka nchini Uganda na Tanzania waliompatia taarifa ya maendeleo ya utafiti wa mafuta katika bonde la bonde la ufa ya Eyasi Wembere la Ziwa Tanganyika Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 5, 2017. Picha na IKULU 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema Serikali ya Awamu ya Tano imedhamiria kufanikisha utafutaji na upatikanaji wa mafuta yaliyopo katika bonde la Eyasi Wembere na ziwa Tanganyika hapa nchini ili Tanzania ianze kunufaika na rasilimali hiyo.

Mhe. Rais Magufuli amesema hayo leo muda mfupi baada kupokea taarifa ya maendeleo ya utafiti wa mafuta katika maeneo ya bonde la ufa ya Eyasi Wembere na ziwa Tanganyika, iliyowasilishwa na timu ya wataalamu wa Tanzania na Uganda.
Timu hiyo imeelezea uwepo wa viashiria vya uhakika vya kijiolojia vinavyothibitisha kuwepo kwa mafuta katika maeneo ya Senkenke, Mwanzugi na Kining’inila katika bonde la Manonga, Wilaya ya Igunga Mkoani Tabora.
Katika mkutano huo uliohudhuriwa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dkt. Medard Kalemani na Balozi wa Uganda hapa nchini Mhe. Richard Kabonero, timu ya wataalamu hao imesema miamba, uoto na uwepo wa bonde Eyasi Wembere katika mfumo mmoja wa bonde la Afrika Mashariki unaofanana na maeneo mengine yaliyothibitika kuwa na mafuta ni kiashiria muhimu cha kuwepo mafuta.

Kufuatia taarifa hiyo Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali ya Awamu ya Tano ipo tayari kutekeleza shughuli zote zitakazowezesha kupatikana kwa mafuta katika bonde la Eyasi Wembere na ziwa Tanganyika na amewaagiza wataalamu wa Tanzania kuendelea kufanya kazi kwa ukaribu na wataalamu wa Uganda ambao wana uzoefu wa kupata mafuta katika ziwa Albert nchini humo.
Mhe. Rais Magufuli amewashukuru wataalamu wa Uganda wanaoshirikiana na wataalamu wa Tanzania katika kazi hii na amemuomba Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini wa Uganda Bw. Robert Kasande kumfikishia shukrani zake kwa Rais wa Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni kwa ushirikiano anautoa kwa Tanzania katika kufanikisha upatikanaji wa mafuta ya nchini Tanzania.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa