Tone

Tone
Home » » NDIKILO AITUPIA SSRA'KAA LA MOTO'

NDIKILO AITUPIA SSRA'KAA LA MOTO'

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Evarist Ndikilo.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Evarist Ndikilo ametaka Mamlaka ya Udhibiti wa Mifuko ya Jamii (SSRA) kutafuta ufumbuzi wa malalamiko ya wafanyakazi hasa utoaji wa mafao kwa wastaafu.
Pia, Ndikilo alisema SSRA inapaswa kuchukua changamoto zote zilizotolewa na wafanyakazi kwenye sherehe za Mei Mosi ambazo kimkoa zilifanyika viwanja vya CCM Kirumba, kwani wengi walidai baadhi ya mifuko kutoa mafao kidogo.
Akifungua mafunzo ya utoaji elimu kwa wafanyakazi wa halmshauri za Mkoa wa Mwanza jana kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa, Mhandisi Evarist Ndikilo, Kaimu Katibu Tawala Mkoa, Warioba Sanya alisema changamoto za mifuko ya jamii zinapaswa kutafutiwa ufumbuzi kuondoa malalamiko ya wafanyakazi.
“Kumekuwa na malalamiko mengi ya wafanyakazi hasa kwa mifuko ya hifadhi ya jamii, naomba SSRA mfanye jitihada kuhakikisha malalamiko hayo yanakwisha ili watumishi wanapostaafu wapate mafao bila matatizo,” alisema Ndikilo na kuongeza:
“Mifano hai tuliiona kwenye sherehe za wafanyakazi CCM Kirumba, kulikuwa na malalamiko mengi yanayohusu mifuko ya jamii ikiwamo kutoa mafao kidogo kwa wastaafu, hivyo naomba suala hilo litafutiwe ufumbuzi mapema.”
Ndikilo alisema kumekuwa na malalamiko ya utoaji mafao yanayotofautiana, jambo hilo linaibua kero kwa wafanyakazi hivyo ni vyema likatazamwa kwa undani.
“Kama mtafanya jambo hilo mtakuwa mmewasaidia, watumishi wote wa umma watanufaika na mifuko hiyo,” alisema Ndikilo.
Mwelimishaji kutoka SSRA, Sarah Kibonde alisema kumekuwa na tatizo la watu kutokujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii, jambo ambalo ni changamoto kwani idadi ya wanachama ni ndogo.
“Mpaka sasa takriban watu milioni 1.8 ndiyo wamejiunga na mifuko ya jamii, nia yetu ni kuhakikisha tunatoa huduma bora kwa Watanzania, hivyo sote tujiunge na mifuko hiyo kwa faida yetu,” alisema Kibonde.
Chanzo;Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa