Home » » WANANCHI ILEMELA WAOMBA KUJENGEWA KITUO CHA POLISI

WANANCHI ILEMELA WAOMBA KUJENGEWA KITUO CHA POLISI

Mwanza. Kufuatia matukio ya uhalifu kujitokeza mara kwa mara Kata ya Buswelu, wilayani Ilemela, mkoani Mwanza, baadhi ya wakazi wa eneo hilo wameitaka polisi kuwajengea kituo na kuimarisha doria.
Hivi karibuni kata hiyo imekumbwa na matukio ya uhalifu baada ya watu wanaominika ni majambazi, kuvamia nyumba kadhaa na maduka kisha kupora mali mbalimbali.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wakazi wa eneo hilo walisema wamechoshwa na matukio ya uhalifu yanayojitokeza mara kwa mara na kwamba, hivi wanataka polisi kuwajengea kituo.
Mmoja wa wakazi hao, Jackline Ismail alisema anashangaa kitendo cha Serikali kuamua kujenga Makao Makuu ya Wilaya ya Ilemela ndani ya kata yao bila ya kujenga kituo cha polisi.
“Hivi wanashindwa kujenga kituo cha polisi, ukizingatia watu wengi wanahamia huku wilayani?” alihoji Ismail.
Aliomba Serikali kuangalia suala la usalama wao.
Hata hivyo, baadhi ya wakazi wa eneo hilo walienda mbali zaidi na kudai kwamba kituo cha polisi cha Mwatex wanachokitumia kupata huduma kiko mbali na hivyo kupelekea wao kushindwa kupata huduma .
Vivian Mtei,Gerald Joseph pamoja na Mhoja walisema kuwa ni muda sasa wa serikali kuhakikisha wanajenga kituo cha polisi sanjari na kuimarisha doria ya mara kwa mara katika eneo hilo kwa lengo la kudhibiti uhalifu .
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa