Tone

Tone
Home » » Serikali iharakishe ujenzi vyuo vya ufundi

Serikali iharakishe ujenzi vyuo vya ufundi

SERIKALI imeshauriwa kuharakisha mpango wa kujenga vyuo vya ufundi stadi (VETA) kila wilaya nchini, ili kuongeza ajira na kukuza uchumi wa nchi.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Magu, mkoani Mwanza, Bonaventra Kiswaga, alitoa ushauri huo kwenye mahafali ya nane ya wanafunzi 25 waliohitimu elimu ya Ufundi katika Chuo cha Ufundi cha Mt. Joseph Kirumba jijini Mwanza.
Kiswaga alisema upo umuhimu kwa serikali kutenga fedha za kutosha katika kufikia malengo hayo, kwani hiyo itachangia maradufu ukuaji wa uchumi.
“Mpango uliopo wa serikali kujenga vyuo vya ufundi stadi kila wilaya ni mzuri katika maendeleo ya Watanzania, iwapo utatekelezwa ipasavyo.
“Kwa hiyo, naishauri serikali itumie fedha zake za ndani na zile za wahisani kujenga vyuo vingi vya ufundi nchini, maana hiyo itaongeza soko la ajira na kukuza uchumi wa wananchi wetu,” alisema Kiswaga.
Pia aliupongeza uongozi wa Chuo cha Ufundi Mt. Joseph kinachomilikiwa na Kanisa Katoliki Kirumba, kwa mikakati yake ya utoaji elimu ya ufundi stadi kwa vijana.
Kuhusu wahitimu, aliwataka vijana hao kuwa na malengo ya kujiajiri na si kuajiriwa.
Awali, akisoma risala ya chuo hicho, Mkuu wa Chuo hicho, Sister Benisia Symphorian alisema wanakishukuru Chuo cha VETA Mwanza kwani kimekuwa kikiwasadia vitu mbalimbali.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa