Clement Mabina
Habari kutoka ofisi ya Kamanda wa Polisi mkoani hapa zimeeleza kuwa watuhumiwa hao walikamatwa kutoka maeneo mbalimbali ya Kata ya Kisesa kwa ajili ya kuhojiwa.
“Zaidi ya watuhumiwa 10 tunawashikilia hadi sasa kwa ajili ya mahojiano. Hadi jana (juzi) mchana tulikuwa nao watuhumiwa saba,” alisema afisa mmoja wa jeshi hilo kwa sharti la kutotajwa jina gazetini.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Valentino Mlowola, hakupatikana ofisini kwake wala kwa njia ya simu yake ya mkononi kuzungumzia suala hilo.
Mara zote simu yake iliita bila kupokelewa na hata alipoandikiwa ujumbe mfupi wa simu ya mkononi (sms) hajajibu.
Katika hatua nyingine, Katibu wa CCM Wilaya ya Magu, Isack Zablon, alisema bado ofisi haijapata taarifa rasmi kuhusu majina ya viongozi wa kitaifa wa chama na serikali watakaohudhuria mazishi ya Mabina yaliyopangwa kufanyika kesho.
“Bado sijapata taarifa kuwa ni viongozi gani wa kitaifa watakaohudhuria kwenye mazishi. Sasa hivi tupo kwenye misa,” alisema Zablon.
Mabina, ambaye alikuwa Diwani wa Kata ya Kisesa, wilayani Magu, aliuawa Jumapili wiki iliyopita, majira ya asubuhi baada ya kushambuliwa na wanakijiji akidaiwa kumuua kwa risasi mtoto mwenye umri wa miaka 12 kutokana na mgogoro wa ardhi baina yake na wakazi wa kijiji hicho.
CHANZO:
NIPASHE
0 comments:
Post a Comment