Mwanamke
mmoja mkazi wa kijiji cha Kisaba katika kisiwa cha maisome wilayani Sengerema
Mkoani Mwanza amejifungua mtoto wa ajabu akiwa hana sehemu za siri hali ambayo
imesababisha kutojulikana jinsia yake.
Mwananmke
huyo anayejulikana kwa jina la Gaundesin Sebastiani (30) amejifungua kichanga
hicho juzi majira ya saa 4 asubuhi katika zahanati ya AICT Kisaba
kisiwani humo.
Mama
huyo anasema alianza kujisikia kuumwa tumbo majira ya asubuhi na hivyo kuamua
kwenda katika zahanati hiyo kisha kijifungua kichanga hicho chenye uzito wa
kilogramu 3, huku kikiwa hakina sehemu za siri kama anavyoelezea.
Kwa
upande wake muuguzi wa zamu wa zahanati hiyo aliyetoa huduma kwa mzazi huyo
Fidesia Marco anazungumzia mazingira ya kuzaliwa kwa kichanga hicho pamoja na
taratibu za kumpeleka katika hospitali ya wilaya ya sengerema..
Diwani
wa kata ya Maisome, Mazabari Mtanzania anasema tayari mzazi huyo na kichanga
chake jana wamepelekwa katika hospitali ya wilaya ya Sengerema kwa uchunguzi
zaidi
0 comments:
Post a Comment