Home » » DC Ukerewe: Serikali inatumia pesa nyingi kulinda mitihani isiibiwe

DC Ukerewe: Serikali inatumia pesa nyingi kulinda mitihani isiibiwe

IMEELEZWA kuwa  kwa zaidi ya  miaka  23 iliyopita  serikali inatumia gharama  kubwa  kulinda mitiani  kufuatia  baadhi ya  maafisa  wenye dhamana kujiusisha na  wizi wa mitiani.

Mkuu wa wilaya  ya Ukerewe, Mwanza  Mery Tesha   amesema hayo jana  wakati anafungua semina  elekezi ya walimu walioteuliwa kusimamia mtiani  wa taifa  wa darasa la saba mwaka  huu  katika wilaya  hiyo.

Alisema    kwa  miaka zaidi ya 23 iliyopita  tangu tatizo hilo la wizi wa mitiani  limejitokeza  linaendelea kughalimu fedha  nyingi  badala ya   kuzielekezwa  katika huduma nyingine za kijamii.

Akifafanua  alisema  wakati wa  kipindi cha miaka ya nyuma  mitiani  hasa ya  elimu ya  msingi, Sekondari na hata  ya vyuo  ilifanyika  chini ya  viongozi  wa ngazi hizo  tofauti na  ilivyo sasa.

Kufuatia  hali  hiyo ameitaka  jamii nzima  hasa  maafisa wenye dhamana  kuacha   vitendo hivyo  kwa sababu mbali ya  kupoteza  fedaha nyingi  za  umma pia  vinazalisha  wataalumu  wasiona sifa.

Afisa elimu ya msingi wa  wilaya hiyo  Fidelis  Munyogwa  alisema  jumla ya wanafunzi 8,969   kati yao  wasichana  4,508 wanatarajia  kufanya mtiani wataifa wa darasa la saba  mwaka huu  kukiwa na ongezeko la  wanafunzi 441 ikilinganishwa na mwaka jana.

Alieleza kuwa  mwaka uliopita  wa 2012  wanafunzi  8,538  walifanya  mtiani huo huku wengine   171  sawa na  asilimia 2.5 walishindwa  kufanya mtiani  huo  kwa sababu ya  utoro.
Hata  hivyo alisema  kiwango cha  ufaulu   wa wanafunzi katika wilaya  hiyo  bado kipo chini   kwasababu ya changamo nyingi   ikiwemo  tatizo la  wanafunzi wengi  kuwa katika chumba kimoja.

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa