Tone

Tone
Home » » BODI YA FILAMU NCHINI YAWATOA GIZANI ZAIDI YA WASANII 300 WA FILAMU MKOANI MWANZA.

BODI YA FILAMU NCHINI YAWATOA GIZANI ZAIDI YA WASANII 300 WA FILAMU MKOANI MWANZA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Zaidi ya wasanii 300 wa filamu mkoani Mwanza, jana wakifuatilia mafunzo kuhusu weledi wa sanaa ya filamu kutoka kwa mkufunzi, Richard Ndunguru, wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam.

Mafunzo hayo ni ya siku tatu ambapo yameandaliwa bure na Bodi ya Filamu nchini, yalianza juzi Novemba 10 na yatafikia tamati leo Novemba 12,2016 ambapo washiriki watakabidhiwa vyeti na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella.

Wasanii, waongozaji pamoja na waandishi wa filamu wamepatiwa mafunzo hayo ili kuboresha kazi zao ikiwemo kuzingatia kazi zenye maadili na maudhui ya mtanzania na zaidi kutambua haki zao ikiwemo hakimiliki za kazi zao na namna ya kuuza kaziuza kwa faida.
Na BMG
Mkufunzi, Richard Ndunguru, kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam, akiwasilisha mada jana kwenye mafunzo ya sanaa ya filamu mkoani Mwanza.
Washiriki wa mafunzo ya sanaa ya filamu mkoani Mwanza
Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo wameishukuru Serikali kupitia Bodi ya Filamu nchini kwa kuwafikishia mafunzo hayo bure na kwamba yatawasaida kuboresha kazi zao na kulifanya soko la filamu mkoani Mwanza kukua.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa