Tone

Tone
Home » » Madai haya ni zaidi ya Ukristo na Uislamu

Madai haya ni zaidi ya Ukristo na Uislamu

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

  Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania , Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete. 
Na Padri Privatus Karugendo

Kwa ufupi
Huyu aliandika akitetea hoja yake kwa takwimu, hata waliomfuatia nao walimjibu kwa takwimu. Hivyo hawa wote hawawezi kuwa wapumbavu kwa wanayoyaamini.
Hivi karibuni, mwandishi mmoja aliandika akihoji hatua ya Rais Jakaya Kikwete kuwateua Waislamu kushika wizara nyeti zote.
Huyu aliandika akitetea hoja yake kwa takwimu, hata waliomfuatia nao walimjibu kwa takwimu. Hivyo hawa wote hawawezi kuwa wapumbavu kwa wanayoyaamini.
Ni vigumu kusema ni upumbavu au siyo upumbavu kila mtu kushikilia hoja yake. Inategemea mtu analiangalia hili kutoka kona ipi na kwa lengo lipi.
Kwa maoni yangu mimi, tatizo lenyewe ni kubwa zaidi ya ndugu hawa wote wanavyoliona. Nina imani kwamba hawa watatu waliojitokeza kuliongelea suala la udini katika Serikali wana wafuasi wao.
Wote wanatoa ushahidi kwamba jambo hili linaongelewa mitaani. Ni kweli linaongelewa, lakini ukweli ni kwamba jambo ni zaidi ya Ukristo na Uislamu.
Hata kama Rais Kikwete, angejitahidi kulinganisha uteuzi wa Wakristo na Waislamu, bado Wahaya wangekuja juu kwamba Wanyakyusa ni wengi zaidi katika Serikali yake.
Angejaribu kutoa haki sawa kwa makabila yote, bado watu warefu wangelalamika kwamba watu wafupi wamependelewa zaidi! Kama angefanikiwa kutoa haki sawa kwa warefu na wafupi, basi suala la sura lingejitokeza.
Wenye sura “nzuri” wangelalamika kwamba, amewapendelea watu wenye sura “mbaya” Kama tunakumbuka wakati wa kampeni kuna baadhi ya watu walikuwa wanasema kwamba mgombea Jakaya Kikwete, alikuwa na sura ya kuvutia kuliko wagombea wengine.
Walimpenda siyo kwa sababu nyingine, ni kwa vile sura yake ni nzuri! Hivyo na sura inaweza kuwa hoja!
Tuliangalie kwa upana zaidi
Hoja yangu ni kwamba hili la kuwapendelea Waislamu au Serikali za awamu nyingine kuwapendelea Wakristo, linakwenda mbali zaidi ya Ukristo. Ni lazima kuliangalia kwa upana zaidi.
Malalamiko haya yanayojitokeza na ambayo yataendelea kujitokeza kila mara ni ushahidi wa kutosha kwamba bado hatujafanikiwa kuwa na mfumo wa kutusaidia kulenga pamoja kama Taifa

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa