Tone

Tone
Home » » WATENDAJI WANAOTUHUMIWA KUIBA MILIONI 43 WAMETIWA MBARONI, MWANZA.

WATENDAJI WANAOTUHUMIWA KUIBA MILIONI 43 WAMETIWA MBARONI, MWANZA.

Mkuu wa mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo ameamuru maafisa watendaji wawili, akiwemo wa kata ya Sangabuye katika halmashauri ya manispaa ya Ilemela wanaotuhumiwa kwa ubadhirifu wa zaidi ya shilingi milioni 40 zilizotokana na mauzo ya viwanja vya biashara na makazi katika kijiji cha Sangabuye kuwekwa mahabasu wakati uchunguzi dhidi yao ukiendelea kufanyika.
Maofisa watendaji waliokamatwa na polisi wakati wa mkutano wa hadhara ulioitishwa na mkuu wa mkoa wa Mwanza Magesa Mulongo baada ya kulalamikiwa na wakazi wa kijiji cha kayenze kwa ubadhirifu wa shilingi milioni 43 ni afisa mtendaji wa mtaa wa kayenze Musa Zablon Bujiku pamoja na aliyekuwa afisa mtendaji wa kata ya Sangabuye Damas Ntenganija. Kwa sasa Ntenganija hana kituo maalum cha kazi baada kushushwa madaraka hadi kubakia afisa mtendaji wa mtaa- hata hivyo hajapangiwa rasmi kituo cha kazi.
Kabla ya mkuu wa mkoa kumuagiza Ocd wa wilaya ya Ilemela kuwatia mbaroni viongozi hao, baadhi ya wakazi wa kijiji cha Kayenze waliwasilisha malalamiko ya kutafunwa kwa fedha hizo, ambapo shilingi milioni tano zilikuwa ni kwa ajili ya uendeshaji wa mradi wa maji kwa kuiomba serikali kuwawajibisha viongozi waliohusika na ubadhirifu huo.
Mkuu huyo wa mkoa wa Mwanza pia amesema serikali haitarudi nyuma katika kukabiliana na uharamia unaofanyika ndani ya ziwa Victoria.
 Chanzo:ITV Tanzania
kiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa