Home » » KWIMBA KUANZA KUNYWA MAJI SAFI

KWIMBA KUANZA KUNYWA MAJI SAFI

MBUNGE wa Kwimba mkoani Mwanza, Shanif Mansoor (CCM), amewahakikishia wananchi wa Ngudu na Mhalo kwamba ifikapo Machi wataanza kupata majisafi kutoka Ziwa Victoria.
Alisema kuanzia Juni hadi Oktoba, wakazi wa kata mbalimbali ikiwemo Hungumalwa, wataanza kupata umeme kupitia Mpango wa Umeme Vijijini (REA).
Mansoor alisema hayo juzi alipofanya ziara ya ukaguzi miradi ya maendeleo ikiwemo kuzungumza na waganga wa jadi ambapo aliweka wazi kwamba tayari miradi hiyo ipo kwenye utekelezaji.
Mradi wa maji ni ahadi iliyotolewa hivi karibuni mjini Ngudu na Waziri wa Maji, Profesa Jumanne Maghembe mbele ya Rais Jakaya Kikwete.
Alitaja maeneo yatakayopatiwa umeme kuwa ni Mwang’halanga, Mhalo, Igogwa, Hundi, Lwande, Kikubiji na Mwamhala.
Kwa mujibu wa mbunge huyo, kukamilika kwa miradi hiyo kutasaidia wakazi wake kuanzisha miradi mbalimbali ya maendeleo kwa kuwa sasa maeneo mengi hayana umeme wala maji.
Aliahidi pia kuendelea kuchimba na kukarabati visima vya maji na mabwawa kwa fedha zake ili kupunguza adha ya maji inayowakabili huku akibainisha kwamba amechimba na kukarabati visima 30.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa