BODI ya Pamba nchini imeweka mikakati
mbalimbali ya kudhibiti viwango vya ubora wa zao hilo ili kuhakikisha
kuwa Pamba inayozalishwa na wakulima inapata bei nzuri na soko la uhakika
ndani na nje nchi.
Miongoni mwa mikakati hiyo ni pamoja na kuanzisha miradi
mbalimbali ya kuelimisha wakulima juu ya kilimo bora
cha zao hilo, pamoja na Makampuni yanayojihusisha na kilimo
cha mkataba kutoa mbegu bora, pembejeo mbalimbali, ushauri wa kitaalamu pamoja
na vifungaishio
Akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa zao hilo
mkoani Singida, mwakilishi wa Bodi ya Pamba bwana Epaphra Swai amesema lengo la
mradi huo ni kuhakikisha zao hilo linamkoamboa mkulima.
Mgeni rasmi katika ufunguzi wa mkutano huo mkuu wa
mkoa wa Singida Dokta Parseko Kone amesema ni vyema hatua hiyo
iende pamoja na kutafuta wawekezaji katika sekta ya kuchambua pamba
Mbali na changamoto ya ubora, wastani wa
uzalishaji wa Pamba mkoani Singida ni Kg 350 kwa ekari, tofauti na
kiwango cha kitaifa cha Kg 1500.
0 comments:
Post a Comment