Home » » Rocky City Marathon yazinduliwa.

Rocky City Marathon yazinduliwa.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, 
Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel 
akikata utepe kuashiria uzinduzi wa awamu ya tano
 ya Mbio za Rock City Marathon 2013, 
leo Jijini Dar es Salaam. Pembeni yake ni Kaimu 
Mkurugenzi wa Kampuni ya Capital Plus International (CPI), 
Dkt. Hellen Otaru Okoedion. Mbio hizo
 zinazoandaliwa na kuratibiwa na CIP 
zinatarajiwa kufanyika  mkoani 
Mwanza tarehe 27 Oktoba, mwaka huu.


Katibu Mkuu wa Chama cha Wanariadha Tanzania,
 Bw. Suleiman Nyambui (katikati) akimueleza jambo 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, 
Vijana, Utamaduni na Michezo, Prof. Elisante Ole Gabriel
 baada ya uzinduzi wa awamu ya tano ya mbio za
 Rock City Marathon leo Jijini Dar es Salaam. 
Anayeshuhudia ni Mkuu wa Masoko na 
Uhusiano wa Precision Air, Bibi Linda 
Chiza ambao ni mmoja wa wadhamini wa mbio hizo.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, 
Vijana, Utamaduni na Michezo,
 Prof. Elisante Ole Gabriel (katikati aliyevaa suti nyeusi)
 akiwa katika picha ya pamoja na waandaaji, 
wadhamini na watendaji wa Baraza la Michezo 
Tanzania wakati wa uzinduzi wa awamu ya tano 
ya mbio za Rock City Marathon leo Jijini Dar es Salaam.
 Wa pili kulia ni Mwenyekiti wa Baraza la Michezo
 la Taifa (BMT), Bw. Dioniz Malinzi, wa pili ni
 Kaimu Mkurugenzi wa Kampuni ya Capital 
Plus International, Dkt. Hellen Otaru Okoedion na
 wa kwanza kushoto ni Katibu Mtendaji 
wa BMT, Bw. Henry Lihaya. Mbio hizo 
zinazoandaliwa na kampuni ya Capital Plus
 International zinatarajiwa kufanyika mkoani 
Mwanza tarehe 27 Oktoba, mwaka huu.
(Picha zote na Concilia Niyibitanga)

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa