Tone

Tone
Home » » ALIYETANGAZWA KUKIHAMA CHAMA CHA MAPINDUZI WAKATI WA UJIO WA LOWASSA, APEWA DHAMANA YA KUTANGAZA UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM MKOA WA MWANZA

ALIYETANGAZWA KUKIHAMA CHAMA CHA MAPINDUZI WAKATI WA UJIO WA LOWASSA, APEWA DHAMANA YA KUTANGAZA UZINDUZI WA KAMPENI ZA CCM MKOA WA MWANZA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


 MARA baada ya Cha cha mapinduzi CCM kuzinduliwa kampeni zake za uchaguzi kitaifa ndani ya jiji la Dar es salaam viwanja vya Jangwani, mbio za kampeni sasa zinaendelea kwenye mikoa mbalimbali hapa nchini ambapo mkoa wa Mwanza unategemea kufanya uzinduzi wake kesho (jumatano) ya tarehe 26 August 2015 na mgeni rasmi  anatazamiwa kuwa Mjumbe wa NEC Livingstone Lusinde maarufu Kibajaji ambaye ni mbunge wa Mtera.

Kwa mujibu wa Katibu uenezi wa CCM Mkoa wa Mwanza Simon Mangelepa amesema kuwa uzinduzi huo utafanyika katika viwanja vya Mbugani wilayani Nyamagana kuanzia saa sita mchana hadi saa 12 jioni ambapo maandalizi yote yamekwisha kamilika.

Ameongeza kuwa Mhe. Lusinde ataambatana na mwenyeji wake katibu wa CCM Mkoa wa Mwanza pamoja na viongozi wengine waandamizi wa chama hicho kuwatambulisha madiwani wateule 19 wa wilaya ya Nyamagana na 18 kwa wilaya ya Ilemela
 Majimbo mengine yaliyoalikwa kwenye uzinduzi huo ni pamoja na Magu, Sengerema, Ukerewe, BOFYA PLAY KUSIKILIZA.

Vipi kuhusu taarifa zilizoenezwa kipindi cha ziara ya mgombea urais kwa tiketi ya CHADEMA (UKAWA) Edward Lowassa zikimtaja katibu huyo mwenezi mkoa wa Mwanza (Simon Mangelepa) pamoja na mwenyekiti wake Anthony Diallo, kuwa wangekihama chama hicho na kujiunga CHADEMA ikiwa ni pamoja na kutambulishwa kwenye mkutano uliopita wa kuomba wadhamini kanda ya ziwa zinaukweli kiasi gani. Bwana Mangelepa alijibu ..
 
KWA HISANI YA GSENGO BLOG 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa