Tone

Tone
Home » » MIUNDOMBINU INAWAKIMBIZA WANAFUNZI WA UTALII

MIUNDOMBINU INAWAKIMBIZA WANAFUNZI WA UTALII

UBOVU wa miundombinu na wataalam katika vyuo vya Utalii nchini, unachangia kuikosesha serikali mapato kutokana na wanafunzi kutoka mataifa mengine kushindwa kuja kusoma wakihofia ubora wa mafunzo unaotolewa.
Kauli hiyo imetolewa mwishoni mwa wiki iliyopita na Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Wanayama pori mkoani Mwanza, Lowaeli Damalu wakati wa mahafali ya chuo hicho jijini hapa.
Alisema miundombinu mibovu katika chuo hicho umesababisha muhula wa mafunzo mwaka 2014/15 wanafunzi kutoka Sudan na Msumbiji kushindwa kuwasili kutokana na kuwepo ubovu wa miundombinu.
Alisema wananchi wanafahamu sheria za wanayama pori na utuzaji wa mazingira lakini wanakiuka sheria hizo kitendo kinachoongeza uharibifu wa misitu na uwindaji haramu.
  Chanzo;Tanzania Daima
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa