Tone

Tone
Home » » MDEE AMKARIBISHA WARIOBA CHADEMA

MDEE AMKARIBISHA WARIOBA CHADEMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Halima Mdee akihutubia kwenye uwanja wa Getrude Mongela mjini Nansio, Ukerewe
MWENYEKITI wa Baraza la Wanawake la CHADEMA (BAWACHA), Halima Mdee, amewakaribisha katika chama hicho, wajumbe wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba chini ya Jaji mstaafu Joseph Warioba, akisema wanawathamini kama wafalme kwa kazi nzuri waliyoifanya.
Mdee alitoa ukaribisho huo juzi wakati akizungumza na umati mkubwa wa wananchi katika mkutano wa hadhara, uliofanyika kwenye uwanja wa Getrude Mongela mjini Nansio, wilayani Ukerewe.
Alisema kuwa Warioba na wazee wenzake kwenye tume yake, wamelitumikia Taifa kwa uadilifu mkubwa bila kukwapua fedha za Umma, na kwamba walifanya kitendo cha uadilifu mkubwa cha kuweka kando maslahi ya vyama vyao ili kuhakikisha maoni ya wananchi zanazingatiwa kwenye rasimu.
“CHADEMA na UKAWA tunawatamani kweli, kama chama chao hakiwapendi na wao hawataki kuhama, wakifukuzwa yaani kwetu watapokelewa kama wafalme… karibuni sana,” alisema Mdee huku akishangiliwa.
Kuhusu katiba mpya inayopendekezwa, Mdee alisema kuwa muungano wa wanawake wanaharakati wa Katiba, umewasaliti wanawake nchini kwa tamko la kwamba katiba hiyo imezigatia maslahi ya wanawake kupata haki zao.
Mdee alisema kuwa miongoni mwa wanawaharakati waliotoa tamko hilo ni wanawake aliokuwa akiwaheshimu toka akiwa mdogo akiamini kuwa ni watetezi wa wanawake lakini kwa kitendo chao cha kushindwa kusimamia maslahi ya wanawake wenzao, kimemsikitisha sana.
Akiwa ameambatana na Makamu Mwenyekiti, Hawa Mwaifunga, Katibu Mkuu, Grace Tendega, Naibu Katibu, Kunti Yusuph na Katibu Uenezi wa BAVICHA, Edward Simbeye, Mdee alisema kuwa hoja ya uwakishi sawa 50 /50 kwenye nafasi za uongozi si kipaumbele cha wanawake wa Tanzania.
Alisema kuwa wanachotaka ni katiba kuhakisha upatikanaji wa huduma muhimu ikiwemo afya, elimu bora kwa watoto wao na fursa za kiuchumi kuwa ni haki yao kikatiba.
“Wanasema kuwa wanaipongeza katiba pendekezwa kwa kutoa fursa ya 50 /50 kwenye nafasi za uongozi, hivi kweli hiki ni kipaumbele cha wanawake?
Inamsaidiaje mwanamke wa kijijini. Wanawake wanataka katiba iwahakikishie upatikanaji ya huduma muhimu na fursa muhimu na wakizikosa waweze kwenda kuzidai mahakamani,” alisema.
Naibu Katibu wa BAWACHA, Kunti Yusuh, aliwataka wanawake wa CCM kuacha kujiita wao ni Umoja Wanawake wa Tanzania (UWT) kwa kile alichodai si wanawake wote wa Tanzania wako kwenye chama hicho.
“Wameshindwa kutuletea huduma bora za afya, wameshindwa kutuhakikishia elimu bora kwa watoto wetu, katiba haituelezi vipi tutadai haki ya kupewa fursa zetu kiuchumi, wanatuambia tutapewa nafasi 50/ 50 kwenye uongozi, nani kasema hiki ni kiaumbele cha wanawake? Alihoji.
Mbunge wa Ukerewe, Salvatory Machemli (CHADEMA), alisema kuwa kwenye jimbo hilo hakuna mzazi atakayechangishwa mchango wa ujenzi wa maabara kama ilivyoagizwa na Rais.
Alisema kuwa maabara hizo zitajengwa na halmashauri ya wilaya kwa fedha za kodi inayokusanywa kutoka kwa wananchi.
Chanzo:Tanznia Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa