Tone

Tone
Home » » WANAWAKE 600 KUPEWA ELIMU YA UJASIRIAMALI

WANAWAKE 600 KUPEWA ELIMU YA UJASIRIAMALI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
ZAIDI ya wanawake 600 mkoani Mwanza, wanatarajiwa kupata elimu juu ya ujasiriamali, usimamizi wa fedha, uwekaji akiba pamoja na mafunzo ya afya bora katika viwanja vya Mwaloni Kirumba Septemba 4 na 5 mwaka huu.
Kina mama na vijana kutoka Wilaya za Magu, Ilemela, Misungwi na Nyamagana, wanatarajiwa kushiriki katika kampeni hiyo itakayotolewa na taasisi ya Angels Moments ya jijini Dar es Salaam.
Akizungumza kwa njia ya simu kutoka jijini Mwanza jana, Mkurugenzi wa Taasisi ya Angels Moments, Naima Malima, alisema kampeni hiyo inalenga kuwajengea uwezo na ujuzi wa kusimamia fedha zao kwa lengo la kunyanyua uwezo wao wa kiuchumi pamoja na familia zao.
Naima, alisema kampeni hiyo imeanzia mkoani Mwanza kwa kutambua fursa zilizopo mkoani humo, hivyo wanawake wa Mwanza watapewa elimu ya msingi ya kibiashara na kuchochea namna ya kuchangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo ndani na nje ya Mkoa wa Mwanza.
“Kwa kushirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii pamoja na taasisi ya Wama, tunatarajia kuwafikia wanawake wa vikundi vyote vya kijamii, Saccos, Amcos, Vicoba na makundi mengine ya kijamii yanayojihusisha na wajasiriamali na hivyo kampeni hii itawawezesha kujiongezea uwezo wa kupata wateja wa bidhaa na huduma zao na kujitangaza zaidi,” alisema Naima.
Aidha, alisema pamoja na Mkoa wa Mwanza, kampeni ya Mwanamke na Uchumi pia itafanyika Tanga, Kigoma, Dodoma, Pwani, Ruvuma na Lindi kuanzia mwishoni na mwanzoni mwa Septemba hadi Januari mwakani.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa