Tone

Tone
Home » » HATIMAYE MAMA SHUJAA WA CHAKULA 2014 AKABIDHIWA ZAWADI YAKE WILAYANI UKEREWE MWANZA

HATIMAYE MAMA SHUJAA WA CHAKULA 2014 AKABIDHIWA ZAWADI YAKE WILAYANI UKEREWE MWANZA


 
Mama Shujaa wa Chakula 2014  Bahati Muriga akitoa neno la Shukurani Baada ya Kukabidhiwa zawadi rasmi zawadi zake Wilayani kwake Ukerewe
Eluka Kibona kutoka Oxfam akimkabidhi ufunguo wa Pikipiki Mshindi wa Mama shujaa wa Chakula
 Mama Shujaa wa Chakula 2014 Bahati Muriga akisaini kupokea zawadi zake kutoka OXFAM kupitia Programu ya GROW, Wekeza kwa wakulima wadogo wadogo Inalipa.
Bwana Hamis Kombo muwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe akitoa salamu za pongezi kwa Mama Shujaa wa Chakula 2014 pia kuwashukuru OXFAM kwa kutoa zawadi hizo.
Bahati Muriga akijaribisha kuiwasha Pikipiki yake Mara baada ya Kukabidhiwa
 Bahati Muriga akifurahia zawadi zake

 Kulwa Kizenga wa kwanza kushoto  na Eluka Kibona kutoka OXFAM  wakimkabidhi zawadi Bahati Muriga
 Mkamiti Mgawe wa kwanza kushoto kutoka OXFAM akiwa na Mama shujaa wa Chakulaa
Zawadi alizopokea Mama Shujaa wa Chakula.

***************


Mshindi wa Maisha Plus/Mama shujaa wa chakula msimu wa tatu 2014 Bahati Jacob Muriga jana alikabidhiwa zawadi nyumbani kwake  Ukerewe. Zawadi hizo ni vifaa vya kilimo vyenye thamani ya shilingi milioni 20 ambapo Bahati Muriga alichagua kununua shamba lenye ukubwa wa ekari 7, pikipiki yenye miguu mitatu aina ya TOYO, vifaa vya kulimo kama vile mbegu, mbolea, mipira ya kumwagilia, watering cane, water pump, spray pump, koleo na dawa za kuondoa wadudu na ukungu, majembe, mundu, engine oil lita 2  na petroli lita 96.
Shindano la Maisha Plus/Mama Shujaa wa Chakula 2014 lilifikia tamati mnamo  tar. 18 May, 2014 ambapo Bahati Jacob Muriga ndiye  aliyeibuka kidedea  wa shindano hilo. Mama shujaa huyu ni mkulima kutoka Nansio, Ukerewe mkoa wa Mwanza na pia ni mwalimu mkuu shule ya Msingi Mhozya. Ni mjane mwenye watoto watatu na hutumia kilimo kama nguzo ya kuhakikisha mahitaji ya kifamilia yanatimizwa.

Hafla fupi ya kumkabidhi zawadi zake Bahati zilifanyika katika Ukumbi wa Afro Beach ambapo watu na wawakilishi mbali mbali kutoka serikalini na mashirika yasiyo ya kiserikali kama vile Kivulini, EMEDO walihudhuria ili  kushuhudia jinsi anavyokabidhiwa zawadi. 

Bw. Kombo, akimuwakilisha mkuu wa wilaya ya Ukerewe alionesha furaha yake kwa mama shujaa kutoka Ukerewe alisema” Ninayo furaha kubwa na kama kiongozi kijana kuona wilaya yetu imetoa mshindi wa shindano kubwa kama hili na kuiweka ukerewe katika historia na  ramani ya nchi kuwa, kumbe nasi tunaweza, najisikia furaha pia kwa ushindi huu kwani toka anaanza huu mchakato wa kuchukua fomu na kuelekea kijiji cha maisha plus nilikua miongoni mwa niliotoa ushirikiano mkubwa kwa kutoa  ruhusa na araka zangu za yeye kushiriki katika shindano hili kwani ni mwalimu huyu”

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa