Home » » VIONGOZI WASIFICHE TATIZO LA 'UNGA'

VIONGOZI WASIFICHE TATIZO LA 'UNGA'

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

VIONGOZI wa serikali  wametakiwa kutokuwa na  kigugumizi  cha  kuitaja  Tanzania  kuwa ni  kinara  katika  usafirishaji wa  dawa za kulevya  katika  nchi  zilizopo  ukanda  wa Jangwa  la  Sahara  na  Afrika  Mashariki,  ili  kuonyesha  uhalisia wa tatizo na  kulitafutia  ufumbuzi.
Mwenyekiti wa Chama  cha  Waandishi wa Habari za Kupiga Vita Dawa za Kulevya  na  Uhalifu   Tanzania (OJADACT), Edwin Soko, alitoa kauli hiyo mjini hapa alipokuwa akijibu  maswali  ya waandishi wa  habari  kutokana na kauli  ya Naibu Waziri  wa  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Kassimu Majaliwa, juu  ya  ongezeko  la  usafirishaji  na matumizi  ya  dawa za kulevya  nchini.
Alisema kama  serikali  na wadau   wengine  ikiwemo na taasisi ya OJADACT kweli wana  nia  ya  kupambana  na  janga  hili, ni wazi  tukubali  kujinyoshea  kidole.
Soko alisema ripoti  mbalimbali   kama  ya  Umoja  wa Mataifa  kupitia  dawati  lake  la  kupambana na mihadarati   (UNODC) ya mwaka 2013, imetaja  Tanzania  kuongoza kwa kusafirisha dawa za kulevya zikiwemo  heroine na cocaine katika  ukanda wa Afrika  Mashariki.
Alisema sababu  kubwa ya tatizo hilo ni Tanzania  kuwa na  sheria  dhaifu  ambazo  kimsingi  zimeshindwa  kupambana  na  biashara  hiyo kama  vile  kutoa  adhabu  ndogo  kwa watuhumiwa.
“Sababu nyingine ya kushamiri kwa biashara hiyo ni kukua  kwa  soko  la  ndani  la  mahitaji  ya  dawa za kulevya, pamoja na  mipaka  ya  Tanzania  kutokuwa na ulinzi wa kutosha katika vituo  vya  kuingilia  wageni  kama  bandari na viwanja vya ndege,” alisema.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa