Home » » UKEREWE WAPONGEZA MFUKO WA JIMBO.

UKEREWE WAPONGEZA MFUKO WA JIMBO.


BAADHI  ya  wakazi  wa wilaya  ya Ukerewe, Mwanza  wamelizishwa  na utendaji wa  mfuko wa jimbo hilo   kipindi hiki tofauti  na  hapo nyuma ambapo akuna  kumbukumbu   miradi iliyotekelezwa  na mfuko huo.

Wakazi hao  walieleza hayo  jana  katika mkutano wa  adhala ulioitishwa  na  mtandao wa  asasi za kirai  wa wilaya  hiyo [Ungonet] na  kuwasilisha  ripoti  yake  ya uchunguzi   ya kupima  ufanisi  wa mfuko huo katika kipindi cha  mwaka 2010/012.

Katibu  wa  Ungonet   Leocadia  Vedastus   aliwaeleza wananchi waliouzulia mkutano huo  katika kijiji cha  Bukongo  kuwa   mbali ya  mafanikio  yaliyopo  pia wamebaini  mapungufu kadhaa  ikiwemo  baadhi ya miradi kutekelezwa chini  ya kiwango .

Akisisitiza  ukubwa wa  tatizo  hilo  mbali ya  kutaka   kamati  ya  mfuko huo ipewa nguvu ya  kisheria  ya kusimamia  shughuri zake  alikwenda mbali zaidi na kutaka  mwandisi  wa ujenzi  wa halmashauri ya  wilaya  hiyo  achunguzwe  ili kubaini kama  ana sifa zinazostaili  kuwa katika nafasi  hiyo.

Akichangia  maoni yake  Padri  Charles  Masaga  wa kanisa katoriki parokia  ya Nansio  alisema   mbali ya  mapungufu  yaliyopo lakini   uongozi wa  sasa wa mfuko  wa jimbo ni vyema ukapongezwa  tofauti na  ilivyokuwa hapo nyuma.

Alisema   katika kipindi hiki  miradi iliyotekelezwa  na fedha ya mfuko huo ikiwemo kituo kipya cha magari , masoko  na miradi  mingine  vinaonekana  hivyo  kuthibitisha  matumizi ya  fedha ya  mfuko huo katika miradi ya kijamii.

Naye  Majuto  Mkama  mbali  ya  kutojua  shughuri za mfuko huo pia alitaka  taarifa ya  kiasi kinacholetwa  kila mwaka na  matumizi  ya  fedha za mfuko  wa  jimbo tangu uanzishwe  hapo mwaka 2005.

Alisema  shughuri hiyo  inayofanyika sasa  hapo nyuma aikufanyika hivyo  imekuwa sababu kubwa ya  wananchi  wengi  mbali ya  kutofaamu shughuri za mfuko huo pia  akuna miradi  iliyotekelezwa kwa fedha ya mfuko huo  kati ya mwaka 2005/09.

Katibu wa  mbunge  wa jimbo hilo   Mathias  Chilebelo  alisema aelewi chochote  juu ya  fedha za  mfuko wa jimbo  zilizoletwa kipindi hicho cha  2005/09 na kuongeza kuwa kati ya  mwaka 2010 hadi sasa  wamepokea na kutumia  sh. Mil  115.3.

Alisema  fedha hizo  zimetumika  kutekeleza  miradi  17 ya  aina mbali mbali  ya kijamii katika sekta za  kiuchumi, elimu, afya , uchukuzi  na  mazingira na kuongeza kuwa  wakati  anapokea ofisi aikuwa na  kumbukumbu ya shughuri za aina yoyote zilizofanyika  hapo nyuma.

Alisema  zipo  sifa na vigezo  vinavyotumika  kutoa  fedha hizo kwa kila  jimbo ikiwemo kigezo cha cha idadi  ya watu  na kuongeza kuwa  jimbo hilo linatakiwa  kupokea sh. Mil. 84 kila  mwaka lakini  fedha wanayopokea  imekuwa chini hapo na kusababisha  miradi  iliyolengwa  kutotekelezwa kwa wakati.  

Ikumbukwe  hapo  mwaka   2010 aliyekuwa mbunge wa  jimbo hilo  kwa tiketi  ya ccm  Getruda Mongera  alishindwa na   Salvatory Machemli  wa  Chadema  katika uchuguzi mkuu  uliopita.

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa