Tone

Tone
Home » » UHABA WA DAWA WAKWAZA HUDUMA ZA AFYA UKEREWE

UHABA WA DAWA WAKWAZA HUDUMA ZA AFYA UKEREWE



na Jovither Kaijage, Ukerewe
IDARA ya Afya wilayani hapa, haijapelekewa dawa na vifaa tiba kwa miezi mitano sasa hali ambayo inasababisha huduma za afya kuendelea kuwa duni.
Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya, Dk. Joseph Odera, alisema hayo jana katika majumuisho ya mafunzo ya siku tano kwa watumishi wa umma yaliyoandaliwa na Mfuko wa Bima ya Afya (NHIF).
Alisema mara ya mwisho idara hiyo kupokea dawa na vifaa tiba kutoka Bohari Kuu ya Dawa (MSD), ilikuwa Mei, mwaka huu na hadi sasa hakuna kilichopelekwa.
Alisema huduma za tiba katika wilaya hiyo, zinakabiliwa na changamoto nyingi, ikiwemo kupata idadi kubwa ya wagonjwa hasa wanaotoka eneo la wilaya jirani ya Bunda, Mara na mwingiliano wa idadi kubwa ya watu wanaotafuta shughuli za uvuvi.
Naye Ofisa Idara ya wananchama wa NHIF Kanda ya Ziwa, Gabuliel Shole, alisema wanachama wa mfuko huo wanakabiliwa na changamoto nyingi, ikiwemo kukosa dawa na vifaa tiba, huku wakikumbana na kauli za kejeli pindi wanapokwenda kupata huduma za tiba katika vituo vya afya na hospitali.
Alisema katika kipindi cha siku tano, wamefanikiwa kuzifikia kata 21 za wilaya hiyo na kutoa mafunzo ya huduma za mfuko huo kwa wanachama 812, wengi wao wakiwa walimu.
Shole alisema wakati wa mafunzo hayo wamekumbana na changamoto hizo zikiwemo za kukosa huduma nzuri na maalumu inayolingana na gharama za fedha wanayokatwa kuchangia mfuko wa NHIF.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa