Tone

Tone
Home » » RC ATOA SIKU 2 KWA SHULE YA SAHARA, MWEKEZAJI

RC ATOA SIKU 2 KWA SHULE YA SAHARA, MWEKEZAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MKUU wa Mkoa wa Mwanza, Magesa Mulongo ametoa siku mbili kwa mwekezaji aliyejenga uzio wa maduka 41 katika shule ya msingi Sahara katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza na uongozi wa shule hiyo kukaa kwa pamoja na kuwasilisha kwake mpango kazi wa uwekezaji katika eneo hilo kwa pande zote mbili.
Mulongo aliyasema hayo jana wakati alipokutana na wajumbe wa Kamati ya Shule ya Msingi Sahara, watendaji wa Jiji la Mwanza na mwekezaji aliyeingia mkataba wa miaka 33 na Jiji la Mwanza, Donald Kahema kujenga uzio wa maduka 41 katika eneo la shule ya msingi Sahara.
Katika mkataba alioingia na Halmashauri ya Jiji la Mwanza, Julai 15, 2008, Kahema ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Glowide Education Centre ya jijini Mwanza, ametajwa kama mwekezaji na mpangaji wa maduka ya uzio wa shule ya msingi Sahara.
Mulongo alisema uwekezaji uliofanywa katika eneo la Sahara, ambalo ni muhimu kwa ukuaji wa uchumi wa Jiji la Mwanza ni wa kutilia shaka kwa madai kuwa ulilenga kuwanufaisha watu wachache wanaojificha kupitia kwenye mgongo wa mwekezaji wa sasa. Alisema Serikali haiwezi kuvumilia hali hiyo.
Awali Kahema ambaye ndiye aliyekuwa mwekezaji wa kwanza kuingia mkataba na Halmashauri ya Jiji la Mwanza, anadaiwa kushindwa kukamilisha ujenzi wa kipande kimoja cha uzio ambacho kilikabidhiwa kwa mwekezaji mwingine kukijenga, huku mwekezaji huyo akilipa fedha kidogo kwa Jiji la Mwanza.
Aidha, mwekezaji, Mwalimu Mkuu Shule ya Sahara Samike Gwanda na wajumbe wa Kamati ya Shule walishindwa kutoa maelezo ya kina juu ya taratibu zilizotumika kujenga uzio wa shule hiyo, ikiwamo kumchukua mwekezaji mwingine, Michael Kisiki kujenga sehemu ya kipande cha uzio huo, hali iliyokiuka taratibu za ujenzi.
Kwa upande wake, Kahema aliyeingia makubaliano ya kuwekeza katika eneo hilo kwa muda wa miaka 33 kwa gharama ya Sh bilioni 1.6, alisema alifuata taratibu na sheria za ujenzi wa uzio huo kwa kuandika barua kwa uongozi wa shule hiyo na kupewa kibali na uongozi wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza.
 CHANZO ; HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa