Tone

Tone
Home » » MFANYABIASHARA MAARUFU MWANZA AGIZWA KUWASILISHA NYARAKA ZA UJENZI JENGO LA GHOLOFA MWALO WA KIRUMBA.

MFANYABIASHARA MAARUFU MWANZA AGIZWA KUWASILISHA NYARAKA ZA UJENZI JENGO LA GHOLOFA MWALO WA KIRUMBA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, John Wanga (watatu kulia) akitoa maelezo kwa Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Manju Salum Msambya (mwenye kofia katikati) juu ya ukarabati wa dhalula wa barabara inayoelekea Soko la Kimataifa la Mwalo wa Kirumba baada ya kuharibika vibaya na mvua zilizonyesha Desemba 22 mwaka jana huku Diwani wa Kata ya Kirumba, Alex Ngussa(wa kwanza kulia) akisikiliza kama walivyokutwa eneo la tukio.

 Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, John Wanga (wa kushoto) wakiteta jambo na Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Manju Salum Msambya (mwenye kofia katikati) juu ya ukarabati wa dhalula wa barabara inayoelekea Soko la Kimataifa la Mwalo wa Kirumba baada ya kuharibika vibaya na mvua zilizonyesha Desemba 22 mwaka jana huku Diwani wa Kata ya Kirumba, Alex Ngussa(wa tatu kushoto) akisikiliza kama walivyokutwa eneo la tukio.


NA PETER FABIAN, MWANZA.

MKUU wa Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza, Manju Salum Msambya, amemuagiza mfanyabiashara maarufu Jijini Mwanza, Kitano Chacha, kuwasilisha vibali na nyaraka ambazo zinaonyesha uhalali wake kuendelea kujenga ghorofa  zaidi ya saba eneo la Mwaloni Kirumba huku akiwa ndani ya mita 60 kinyume na sheria za mazingira.
 
Msambya alitoa agizo hilo mwishoni mwa wiki wakati alipofika eneo la Mwaloni kujionea uharibifu wa barabara inayoelekea Soko la Kimataifa la Mwaloni Kirumba uliosababishwa na mvua zilizonyesha mfululizo tangu Desemba 22 mwaka jana na kusababisha athari kwa watumiaji wa barabara iendayo Soko la Kimataifa la Kirumba kutopitika kirahisi ikiwemo magari makubwa ya mizzigo kunasa kwenye tope.
 
Akiwa katika eneo hilo la mwaloni huku akiongozana na Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, John Wanga, alipokea baadhi ya malalamiko ya wananchi na wafanyabiashara juu ya kero ya barabara hiyo kutopitika kirahisi pia kudaiwa uharibifu huu pia kuchangiwa na mfanyabiashara Kitano kwa kumwaga vifusi vya mchanga ambao baada ya mvua kunyesha zikawa tope.
 
“Tayari tumekubaliana na Mkurugenzi wa Manispaa, Wanga, kuanza kuifanyia matengenezo ya dhalula wakati pia tukisubilia mvua ziishe na hatua za ukaguzi zilizofanywa na wataalam wa Wizara ya TAMISEMI waliofika kufanya tathimini ya uharibifu ulitokana na mvua zilizonyesha mfululizo kuanzia Desemba 22 mwaka jana, pamoja na kusubilia ripoti ili kuruhusiwa kufanya ukarabati hali hii inatulazimu kufanya ukarabati wa dhalula,”alisema.
 
Mkuu huyo wa Wilaya alieleza kuwa watu ambao wamejenga katika kandokando ya Ziwa Victoria bila kuzingatia sheria za mazingira, vibali halali na kuamua kujenga kwa jeuri wakitumia fedha zao kupata hati na vibali kinyume kanuni, taratibu na sheria tumeomba mwongozo wa wataalamu wa Mazingira (NEMC) kuja kufanya ukaguzi na kutoa maelekezo.
 
“Hapa Mwaloni kuna jengo la ghorofa zaidi ya saba linajengwa na ujenzi wake ni zege tupu ni mali ya mfanyabiashara Chacha nimemuagiza badala ya kuendelea kujenga alete nyaraka zake za umiliki wa eneo hilo, vibali vya ujenzi na maelezo kwa nini anajenga jengo hilo ambalo ukiliangalia liko ndani ya mita 60 ambazo kisheria ni kosa, pia nasikia anasomba mchanga ili kujaza ziwani ili kupata mita hizo 60 ikibainika tumeomba asifanye hivyo na akikaidi tutachukua hatua ikiwemo na majengo mengine eneo hilo la mwaloni,”alisisitiza.
 
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Manispaa, Wanga alieleza kwamba kutokana na uharibifu wa barabara nyingi za Manispaa kuharibika bado wanaendelea kusubilia ripoti ya wataalamu wa Wizara ya TAMISEMI kuirejesha ili kutuwezesha kufanya ukarabati wake lanini kwa hii ya mwaloni tumeona tuifanyie matengenezo ya dhalula ili kuwezesha kupitika kilahisi.
 
“Barabara hii inakwenda kwenye chanzo kikuu cha mapato ya Manispaa yetu ambacho ni Soko la Kimataifa Kirumba Mwaloni hivyo imetulazimu kufanya ukarabati wa dhalula na tutatumia zaidi ya Sh milioni 5 kwa kutandaza mawe na kicha kuweka moramu, barabara za Sabasaba-Kiseke, Kirumba-Ibanda, Pansiasi-Lumala, Bwiru zinasubilia ripoti ya wataalam wa TAMISEMI, juu ya waliojenga maeneo yenye utata kwenye fukwe za Ziwa Victoria tunasubilia pia watu wa Mazingira waje kufanya ukaguzi na kutoa maelekezo ,”alisema.
 
CHANZO G SENGO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa