na Jovither Kaijage, Ukerewe
SHUGHULI
za maendeleo wilayani Ukerewe, Mwanza zimeanza kukwama baada ya wenyeviti wa
vitongoji kususa kushiriki na hata kuamasisha wananchi kutojitokeza katika
mikutano ya viongozi wakishinikizwa kulipwa posho mbalimbali ikiwamo ya Sensa
ya Watu na Makazi.
Msimamo
huo umedhihirika juzi baada ya mkutano wa hadhara ulioitishwa na mkuu wa wilaya
hiyo katika Kijiji cha Hamkoko kushindwa kufanyika baada ya wenyeviti wa
vitongoji kugoma kualika wananchi.
Habari
kutoka katika kijiji hicho zinasema pamoja na Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ngoma,
Khamis Ndaro, kuwaelekeza wenyeviti wa vitongoji kushiriki kikao cha ndani cha
viongozi wa vijiji viwili vya Hamkoko na Muluseni pamoja na kualika wananchi
kushiriki mkutano wa haadhara, lakini hali ilikuwa tofauti.
Wakieleza
sababu ya kususia shughuli za maendeleo kwa nyakati tofauti, wenyeviti hao
wanataka kulipwa posho ya sh 50,000 kila mmoja ya kushiriki sensa mwaka huu
pamoja na posho ya madaraka ya kila mwezi ya sh 5,000 ambayo haijalipwa zaidi
ya miezi tisa sasa.
Mwenyekiti
wa umoja wa wenyeviti wa vitongoji katika wilaya hiyo, Hussein Hassan, alisema
katika vikao vyao wamekubaliana kutoshiriki shughuli zote za maendeleo hadi
madai yao yatakapotekelezwa.
Mkuu
wa wilaya hiyo, Mary Tesha, alithibisha mkutano huo kutofanyika kutokana na
wananchi kutoalikwa.
Chanzo: Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment