Home » » WALIMU WANNE MBARONI KWA KUANDAA MAJIBU MTIHANI DARASA LA SABA

WALIMU WANNE MBARONI KWA KUANDAA MAJIBU MTIHANI DARASA LA SABA

Na Mwandishi wetu
Walimu wanne  wa Shule ya  Msingi Hamkoko Wilaya hapa mkoani Mwanza  wanashikiwa na polisi  kwa tuhuma ya  kukutwa wakiandaa majibu ya mtihani wa Taifa wa darasa la saba.

Walimu hao walikamatwa na polisi juzi majira ya saa 5.10 asubuhi  nyumbani kwa mmoja wa  watuumiwa hao wakiendelea na harakati za  kuandaa majibu ya mtihani ili kuwasaidia wanafunzi wa shule hiyo.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mwanza , Leberatus  Barlow  amewataja  walimu hao kuwa  ni  Kija  Songoli (30), Jenfrida Edward (28), Merycelina Malisel (25)  na Maliam Kateti (26) ambaye alikuwa Msimamizi wa Mtihani huo katika shule hiyo.

Alisema  mwalimu  Diana  Shishangali  ambaye ni mmoja wa watuhumiwa anatafuta baada ya kutoka ili  aunganishwe na wenzake kwa ajili ya kufikishwa mahakamani.

Kamanda Barlow alisema  walimu hao walikutwa nyumbani kwa  Kija  Songoli  wakiwa na nakala ya  mtihani wa Hesabu, mashine moja ya kufanyia mahesabu, kalamu pamoja na  vipande kadhaa vya kalatasi  vikiwa  tayari vimeandikwa majibu ya mtihani huo vikiwa vimefichwa chini ya godolo.

Alisema  wakati uchuguzi zaidi wa tukio hilo ukiendelea, tayari baadhi ya vielelezo  vimepatika na  vimeandaliwa  ili vipelekwe kwa  wataalamu wa kutambua  miandiko  ili kubaini  aliyeusika na kosa hilo.

Kwaupande wake Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe, Mery Tesha, alisema ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuimarisha ulinzi ili yeyote atakayepatikana kufanya hujuma za kuiba mitihani akamatwena kuchukuliwa hatua kwamujibu wa sheria.
Chanzo: Nipashe

0 comments:

 
Blogs za Mikoa
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Blogs za Mikoa
Proudly powered by Blogs za Mikoa