Tone

Tone
Home » » Uongozi wa Msitu wa Buhindi Sengerema wagawa madawati kwa shule za msingi

Uongozi wa Msitu wa Buhindi Sengerema wagawa madawati kwa shule za msingi

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Untitled
Afisa Elimu Msingi wilaya Sengerema Bw. Juma Mwajombe akikadhiwa madawati.
Na Daniel makaka, Sengerema.
WALIMU wakuu shule za msingi katika kata ya Bupandwa wilaya ya Sengerema mkoa wa  Mwanza wameombwa kutumia vyema madawati yaliyotolewa na uongozi wa  msitu wa Buhindi  kwa lengo la kusaidia kutatua tatizo la madawati katika shule hizo.
 Hayo yamesemwa  na Afisa Elimu ya msingi wilaya ya Sengerema Bw Juma Mwajombe katika sherehe za kukabidhiwa madawati hayo  iliyofanyika katika sherehe za Mei Mosi katika kata ya Bupandwa ambapo  uongozi wa msitu wa Buhindi ulikabidhi madawati 80 katika kata hiyo ambapo yatagawiwa katika shule zote za kata hiyo .
Untitled 1
Diwani wa kata ya  Bupandwa Bw. Masumbuko Bupamba akitoa shukurani baaada ya kukabidhiwa madawati.
Akikabidhi madawati hayo Meneja Msaidizi wa Msitu huo Bw Ernesti Madatta amesema kuwa msitu wa Buhindi umekuwa mstari wa mbele kusaidia jamii hiyo na  itaendelea kutoa misaada katika shule hizo ili kuleta usawa  kwa kuwa jamii hiyo inasaidia kulinda raslimali za msitu huo.
“madwati haya yamegharimu zaidi ya shilingi za kitanzania milioni tatu fedha taslimu na tutaendelea kutoa msaada kwenye jamii zinazotuzunguka,’ amesema Madatta.
Untitled 2
Meneja msaidizi msitu Buhindi  Bw. ERNEST MADATA.
 Bw, Madata aliongeza kuwa sambamba na kukabidhi  madawati hayo pia msitu huo unajenga kituo cha afya  katika kata hiyo pia jengo  la mama na mtoto katika zahanati ya Bupandwa ambapo kila moja itagharimu shilingi milioni sabini pia amewataka wananchi wa kata hiyo kushirikiana vema na msitu huo kuleta ushirikiano wa dhati miongoni mwao.
 Kwa upande wake Diwani wa kata hiyo Bw Masumbuko Bupamba amemshukuru meneja huyo jinsi wanavyosaidia jamii hiyo na amewaomba waendelee na juhudi hizo za kusaidia jamii.
Untitled 44
Msitu wa Buhindi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa