Tone

Tone
Home » » Warsha ya Maafisa Vijana,waratibu wa ukimwi na wadau mbalimbali yafikia siku ya tatu jijini Mwanza

Warsha ya Maafisa Vijana,waratibu wa ukimwi na wadau mbalimbali yafikia siku ya tatu jijini Mwanza


Katibu asasi ya Vijana ya Boys & Girls Bw,Johnson Jacob kutoka Bariadi akionyesha igizo lilikuwa likionyesha wajibu wa Vijana  kwa Familia ikiwamo kuwalinda na kuwapatia mahitaji yao muhimu.
Mtaalamu wa Stadi za Maisha Bw,Robert Semkiwa akiwafundisha waratibu wa ukimwi na maafisa Vijana wanaohudhuria Warsha ya siku tatu inayohusu Stadi za maisha na Afya ya uzazi jinsi ya kukabiliana na Msongo wa Mawazo na njia gani za kutumia kukabiliana nao.
Waratibu wa Ukimwi na maafisa Vijana wakiwa katika mjadala wa pamoja wakipambanua kwa kina stadi mojawapo katika stadi tatu za maisha ya kujitambua leo jijini Mwanza.kundi ili lilikuwa likijadili jinsi ya kukabili mihemko kwani ni  hatua mojawapo kijana anayoipitia katika maisha yake.


Mwakilishi wa Vijana kutoka kamati ya kudhibiti Ukimwi manispaa ya Shinyanga Bw,Rigobert Rwehumbiza akielezea wajibu binafsi kwa kijana kwa washiriki wenzie katika warsha ya siku nne ya stadi za maisha na afya ya uzazi.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Mwanza Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa